Ukikutwa na Samsung Galaxy Note 7 unapigwa faini | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Monday 17 October 2016

Ukikutwa na Samsung Galaxy Note 7 unapigwa faini

Abiria wa ndege wazuiwa kubeba simu za Samsung Galaxy Note 7 wakati wa safari nchini Canada

Idara ya usafiri nchini Canada imetangaza kupiga marufuku ubebaji wa simu za Samsung Galaxy Note 7 kwa abiria wakati wa safari.

Idara hiyo ilitoa maelezo na kutangaza kuchukuwa hatua hiyo kutokana na kesi za ulipukaji wa betri za Galaxy Note 7 zilizoripotiwa kwa kampuni ya Samsung hivi karibuni.

Maelezo zaidi yanaarifu kwamba simu hizo pia hazitoruhusiwa kubebwa ndani ya mizigo yoyote inayopakiwa ndani ya ndege.

Mkuu wa idara ya usafiri aliwatahadharisha abiria wote na kusema kwamba wataweza kutozwa faini ya fedha endapo watakiuka kanuni hiyo.

Mkuu huyo aliongezea kusema kuwa hatua hiyo itasaidia kudhibiti hali ya usalama wa abiria wakati wa safari za ndege ingawaje wamiliki wa simu hizo watakuwa na hali ngumu.

 

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us