ALICHOKISEMA ASKOFU GWAJIMA LEO ALIPOTEMBELEA CLOUDS MEDIA LEO TAR 22 , | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Wednesday 22 March 2017

ALICHOKISEMA ASKOFU GWAJIMA LEO ALIPOTEMBELEA CLOUDS MEDIA LEO TAR 22 ,





Askofu wa kanisa la Ufufuo na uzima Joseph Gwajima 

Dar es Salaam. Askofu wa kanisa la Ufufuo na uzima Joseph Gwajima amezungumza na waandishi wa habari  wa Clouds Media Group  na kusema kilichomfanya afike katika ofisi hizo ni kutoa pole kwa kuwa yeye ni sehemu ya sababu za uvamizi huo.

“Isingekuwa busara watu wavamiwe na mimi ni mhusika mkuu halafu nisije kutoa pole,” alisema

Hatua ya Gwajima imekuja baada ya tukio la kituo hicho kuvamiwa na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akiwa na polisi wenye silaha.

Gwajima amewasilia saa 4:00 asubuhi akiwa na msafara wa magari zaidi ya manne na walinzi wake takribani 30 na alipofika alipokelewa na Mkurugenzi wa vipindi na Uzalishaji Ruge Mutahaba na kufanya mazungumzo na waandishi wa habari  na baadaye na uongozi wa kituo hicho.

Amewataka Clouds kuendelea na kazi zao za kawaida na kutaka suala hilo lisichukuliwe kisiasa huku akikisitiza kuwa Mkuu wa mkoa alikosea.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us