Forbes: Hawa ndio Mabilionea 25 matajiri zaidi Afrika 2017 | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Wednesday 22 March 2017

Forbes: Hawa ndio Mabilionea 25 matajiri zaidi Afrika 2017

Mfanyabiashara kutoka Nigeria Aliko Dangote bado ndiye mtu tajiri zaidi barani Afrika kwa mujibu wa orodha ya mabilionea mwaka 2017 iliyoandaliwa na jarida la Forbes.

Utajiri wa Dangote unakadiriwa kuwa jumla ya $12.2 bilioni.
Kuna mabilionea (wa Dola) 25 mwaka huu barani Afrika, mmoja juu ya 24 waliokuwepo mwaka jana.

Wafanyabiasha kutoka Nigeria Femi Otedola na Abdulsamad Rabiu hawakufanikiwa kuingia kwenye orodha hiyo mwaka huu.

Mtanzania Mohammed Dewji bado ndiye bilionea wa umri mdogo zaidi Afrika, utajiri wake ukikadiriwa kuwa $1.09 bilioni.

Isabel dos Santos kutoka Angola na mfanyabiashara wa mafuta Folorunsho Alakija kutoka Nigeria ndiye mabilionea wanawake pekee katika orodha hiyo mwaka huu.

Bw Dangote Dangote, ndiye mwanzilishi na mwenyekiti wa kampuni ya Dangote Cement inayoongoza kwa kuzalisha saruji Afrika. Anamiliki asilimia 90 ya hisa za kampuni hiyo.
Dangote Cement huzalisha tani 44 milioni za saruji kila mwaka na imepanga kuongeza uzalishaji kwa asilimia 33 kufikia 2020.

Dangote pia anamiliki hisa katika kampuni za chumvi, sukari na unga.
Mohammed Dewji ni afisa mkuu mtendaji wa kampuni ya METL iliyoanzishwa na babake miaka ya 1970. Kampuni hiyo huhusika katika biashara ya nguo, unga, vinywaji na mafuta. Kampuni hiyo huendesha shughuli zake katika zaidi ya mataifa sita barani Afrika.

Mabilionea 25 wa Afrika mwaka 2017:

1. Aliko Dangote, Nigeria

    Utajiri: $12.2 bilioni

2. Nicky Oppenheimer, Afrika Kusini

    Utajiri: $7 bilioni

3. Mike Adenuga, Nigeria

   Utajiri: $6.1 bilioni

4. Johann Rupert, Afrika Kusini

   Utajiri: $6.3 bilioni

5. Nassef Sawiris, Misri

   Utajiri: $6.2 bilioni

6. Christoffel Wiese, Afrika Kusini

    Utajiri: $5.9 bilioni

7. Nathan Kirsch, Swaziland

    Utajiri: $3.9 bilioni

8. Naguib Sawiris, Misri

    Utajiri: $3.8 bilioni

9. Isabel dos Santos, Angola

    Utajiri: $3.1 bilioni

10. Issad Rebrab, Algeria

     Utajiri: $3 bilioni

11. Mohamed Mansour, Misri

      Utajiri: $2.7 bilioni

12. Koos Bekker, Afrika Kusini

      Utajiri: $2.1 bilioni

13. Allan Gray, Afrika Kusini

      Utajiri: $1.99 bilioni

14. Othman Benjelloun, Morocco

      Utajiri: $1.9 bilioni

15. Mohamed Al Fayed, Misri

      Utajiri: $1.82 bilioni

16. Patrice Motsepe, Afrika Kusini

      Utajiri: $1.81 bilioni

17. Yasseen Mansour, Misri

      Utajiri: $1.76 bilioni

18. Folorunsho Alakija, Nigeria

      Utajiri: $1.61 bilioni

19. Aziz Akhannouch, Morocco

     Utajiri: $1.58 bilioni

20. Mohammed Dewji, Tanzania

      Utajiri: $1.4 bilioni

21. Stephen Saad, Afrika Kusini

      Utajiri: $1.21 bilioni

22. Youssef Mansour, Misri

      Utajiri: $1.15 bilioni

23. Onsi Sawiris, Misri

      Utajiri: $1.14 bilioni

24. Anas Sefrioui, Misri

     Utajiri: $1.06 bilioni

25. Jannie Mouton, Afrika Kusini

      Utajiri: $1 bilioni



google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us