Jinsi ya Kuokoa Simu Iliyoingia Maji | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Wednesday 22 March 2017

Jinsi ya Kuokoa Simu Iliyoingia Maji






Unaweza ukawa mwangalifu sana ila, bahati mbaya inatokea na simu zetu zinaingia maji.

Sasa, kwa kuwa simu zisizoingia maji bado ni ghali sana, simu yako ikiingia maji unaweza ukaiokoa kwa kufanya yafuatayo.

Itoe kwenye maji
Izime alafu ilaze kwenye kitambaa laini au tishu nzito alafu toa kava la nyuma na betri (kama unaweza kufungua simu yako)
Pia, ondoa SIM card, memory card, kava za simu uziache zikauke.
Kausha simu kwa ndani kwa kutumia kitambaa laini au tishu nzito. Hakikisha unaikausha haraka iwezekanavyo.
Weka simu ya ndani ya mfuko wa mchele kwa masaa 24. Mchele inanyonya maji.
Angalia kama eneo la kuchomeka chaji na headphone zimekauka. Kama bado, rudia  hatua 4 na 5.
Baada ya masaa 24, jaribu kuiwasha alafu angalia kama ina fanya kazi inavyotakiwa.

Kuna uwezekano kwamba utabidi kuipeleka kwa fundi

Ukiona kwamba haifanya kazi baada ya pitia hatua hizi, bora uipeleke kwa fundi. Ipeleke kwa wakala wa aina ya simu (au mtandao) ya simu yako au kwa duka la kutengeneza vifaa vya umeme linaloaminika.

Ila, kuzuia ni bora zaidi ya tiba. Kwa hiyo, nunua kava ya simu inayozuia maji kuingia kwenye simu.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us