Kumekucha! Bifu la Watangazaji wa Shilawadu na RC Makonda lafikia patamu na limenoga sasa | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 1 April 2017

Kumekucha! Bifu la Watangazaji wa Shilawadu na RC Makonda lafikia patamu na limenoga sasa

Image result for shilawadu


Wakiwa katika Kipindi chao ambacho kilikuwa mubashara kabisa Mtangazaji muongozaji wa Kipindi pendwa na Watanzania wengi hadi Mheshimiwa Rais wetu JPM aitwae Soud Brown amekuwa kila mara akifumba Fumbo huku akicheka mno na mwenzake Kwissa.

Ukiwaangalia zaidi utagundua kuwa kwa yale yaliyowatokea wiki mbili zilizopita utagundua kuwa Kipindi chao Kizima cha leo ni kama vile na wao wameamua kulipiza Kisasi kwa waliyofanyiwa na ' Mvamizi ' Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Paul Christian Makonda.

Mtangazaji Soud Brown amekuwa kila mara akifumba fumbo moja hilo hilo huku akilinogesha na Kiitikio na Mistari iliyopo katika Wimbo maarufu wa Ney wa Mitego wa WAPO huku kila mara akimuuliza mwenzie kuwa ' Je mlango wetu umefungwa? '.

Fumbo lenyewe la Mtangazaji Soud Brown ambalo si Siri kuwa amelielekeza ' makusudically ' kabisa kwa ' adui ' yao na ' mvamizi ' wao Makonda ni kama lifuatalo nalinukuu " Hata wanaovua Viatu na Soksi zao zinanuka Wapo........unasema Wapo.......hata wanaonuka Midomo pia Wapo......unasema Wapo.....Oya Kwissa umefunga mlango lakini?...... Jamani hata wanaonuka miguu wakivua Viatu vyao Wapo.......unasema Wapo......hata wanaonuka Midomo sana Wapo......unasema Wapo......Kaka angalia umefunga lakini mlango? Walinzi wapo gado?

Sasa Kazi imeanza na naomba mlio karibu na hawa Watangazi akina Soud Brown na Kwissa mtusaidie kutuulizia kutoka Kwao kuwa huyo anayenuka Soksi na Miguu akivua Viatu ni nani? Halafu na huyo anayenuka mdomo pia ni nani?

Chokoza wote lakini kamwe usichokoze na kuanzisha vita na Waandishi wa Habari kwani wana mbinu nyingi za kukuchafua, kukumaliza na ikibidi hata kukudhalilisha. Pole sana ' mvamizi ' Mkuu wa Clouds nadhani sasa Vita baina yako na wao ndiyo imeanza na imefika patamu mno.

Kuna Watu wanajua mno kulipiza Visasi hasa kwa waliyofanyiwa au mateso ya kimanyanyaso waliyopata.

Nawasilisha.

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us