Hii hapa siri kubwa kuhusu Yamoto Band kupotea Aslay afunguka. | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Friday 19 May 2017

Hii hapa siri kubwa kuhusu Yamoto Band kupotea Aslay afunguka.

Msanii Aslay ambaye hivi sasa ameanza kufanya kazi peke yake nje ya kundi la Yamoto band amefunguka na kusema kundi hilo hapo katikati walikwama na ndiyo maana walirudi nyuma badala ya kusonga mbele zaidi. 

Aslay anasema kipindi cha nyuma walikuwa wanapata show nyingi sana jambo ambali lilipelekea kuwa na uwezo wa kufanya video kubwa hata nje ya nchi lakini baadaye mambo yalibadilika na kupelekea kufanya video zao hapa hapa bongo. 

"Mimi nafikiri kwamba mipango yetu tu wenyewe, kipindi kile tunatoa ile video ' Madoido' kulikuwa na show nyingi zinaongozana ambazo zilituzuia kwenda kutengeneza video nyingine lakini si unajua tulikuwa tunajenga pia kwa hiyo kifupi ni kama tulijisahau na kuteleza kusema ukweli. Tukarudi tena tukafanya 'Suu' ambayo tuliifanya Zanzibar na tukawa na pesa kabisa ambayo ingetuwezesha kutengeneza video nyingine Afrika Kusini lakini hapo katikati tulifanya vitu fulani mchanganyiko ambavyo siwezi kuvisema vikaturudisha tena nyuma"alisema Aslay 

Mbali na Aslay msanii mwingine kutoka kundi hilo Beka Flavour naye ametoka na wimbo wa peke yake akiwa chini ya menejimenti nyingine. 

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us