Klabu ya Man City yafungiwa Usajili Miaka miwili | KINGAZI BLOG

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Saturday 6 May 2017

Klabu ya Man City yafungiwa Usajili Miaka miwili

KLABU ya Manchester City imefungiwa kwa miaka miwili kusajili wachezaji wa umri chini ya miaka 18 sambamba na kutozwa faini ya Pauni 300,000 na Bodi ya Ligi Kuu England kwa kuvunja sheria ya maendeleo ya vijana.

Uvunjaji huo wa sheria unahusu kufanya mazungumzo na wachezaji wawili wa akademi tofauti kwa ajili ya kuwasajili huku wakiwa wamesajiliwa na klabu nyingine. 

Adhabu hiyo ni sawa na waliyopewa Liverpool mwezi uliopita baada ya kukutwa na hatia ya 'kuiba' mchezaji mwanafunzi wa shule wa Stoke City.

Kufuatia uchunguzi wa Bodi ya Ligi Kuu, ushahidi umepatikana kwa City ambao wamevunja sheria za Ligi.

Kuwasilia na mchezaji wa akademi yoyote akiwa amesajiliwa na klabu yake ya wakati husika ni kosa, ambalo City wamefanya na sasa linawagharimu. 

google+

linkedin

About Author
  • BLOG NAMBA MMOJA KWA MATANGAZO YA AJIRA NA NAFASI ZA KAZI TANZANIA. Soma zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    Gallery

    Popular Posts

    About Us