
Wakosoaji wa mwanamapinduzi, aliyekuwa kiongozi wa Cuba, Fidel Castro, wanaoishi Miami, nchini Marekani, kilomita 200 kutoka ufuo wa Bahari wa Cuba, walifanya maadhimisho ya hadharani kufuatia kutangazwa kwa kifo cha kiongozi huyo.
Wengi wao walihamia Miami baada ya Castro kupindua Serikali yenye ufisadi mkubwa, iliyokuwa ikiungwa mkono na Marekani mwaka 1959.
Wengine wengi waliungana nao baada...