KINGAZI BLOG: BREAKING NEWS

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...
Showing posts with label BREAKING NEWS. Show all posts
Showing posts with label BREAKING NEWS. Show all posts

Sunday, 23 April 2017

RATIBA ZA MITIHANI YA VYUO VYA GRADE A NA DIPLOMA , 2017


THE NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA


Please make sure you have PDF reader installed in your device.

Link 1: DIPLOMA IN SECONDARY EDUCATION EXAMINATION MAY, 2017
TIMETABLE (DSEE) CLICK HERE TO DOWNLOAD

Link 2: GRADE A TEACHER CERTIFICATE EXAMINATION MAY, 2017
TIMETABLE (GATCE) CLICK HERE TO DOWNLOAD

Share these announcements as much as you can.

Source: NECTA Official Website

Thursday, 13 April 2017

MPYA: Hii hapa Orodha ya majina ya Walimu wa Sayansi na vituo vya kazi walivyopangiwa

Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI imetangaza ajira mpya kwa Walimu wa masomo ya Hisabati na Sayansi leo tarehe 12 Aprili, 2017.

Majina ya Walimu yaliyotangazwa yanatokana na tangazo la nafasi ya kazi ya Ualimu lililotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia mnamo tarehe 01 Desemba, 2016.

 

Jumla ya Walimu wapya wapatao 3,081 wakiwemo 1,544 ni wa ngazi ya Shahada na Walimu 1,537 ni wa Stashahada.

 

Walimu hao watatakiwa kuripoti kwenye Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri na baadaye kwenye Shule walizopangiwa kuanzia tarehe 18 Aprili, 2017 hadi tarehe 25 Aprili, 2017. Walimu wote waripoti wakiwa na vyeti halisi vya taaluma vya kidato cha nne (IV) na kidato cha sita (VI), vyeti halisi vya kitaalaam vya kuhitimu mafunzo ya Ualimu ngazi ya Stashahada na Shahada na Cheti cha kuzaliwa.

 

Angalizo :

i. Walimu waliopangiwa vituo ni wa masomo ya Hisabati na Sayansi waliohitimu hadi mwaka 2014/2015.

ii. Kituo cha kazi cha mwalimu ni shule aliyopangiwa na sio makao makuu ya Halmashauri.

 

iii. Mwalimu atakayeripoti na kuchukua posho ya kujikimu na baadae kuondoka atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

 

iv. Walimu wote watakiwa kuripoti katika vituo vyao kuanzia tarehe 18 Aprili, 2017 hadi 25 Aprili, 2017, watakaochelewa nafasi zao zitajazwa na mwalimu mwingine.

 

v. Hakutakuwa na uhamisho ndani ya Mkoa au Halmashauri.

Majina ya Walimu hao yanapatikana katika tovuti ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI ya www.tamisemi.go.tz

 

Imetolewa na:

Katibu Mkuu

Ofisi ya Rais TAMISEMI

==>Orodha ya Walimu wa Shahada wa Ajira Mpya kwa Masomo ya Sayansi na Hisabati.

<<Bonyea hapa kudownload>>

==>Orodha ya Walimu wa Ajira Mpya kwa Masomo ya Sayansi na Hisabati.

<<Bonyeza  Hapa  Kuya Download>>

Saturday, 1 April 2017

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UTEUZI WA WAOMBAJI WA UDAHILI WA KOZI ZA ASTASHAHADA (CHETI) NA STASHAHADA (DIPLOMA) KWA AWAMU YA MACHI/APRILI, 2017 KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017





                                                 BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI
                                                                                             (NACTE)

                                                                                    


TAARIFA KWA UMMA
UTEUZI WA WAOMBAJI WA UDAHILI WA KOZI ZA ASTASHAHADA (CHETI) NA STASHAHADA (DIPLOMA)
KWA AWAMU YA MACHI/APRILI, 2017 KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi liliratibu zoezi la udahili kwa waombaji wa kozi za Astashahada (Cheti) na Stashahada (Diploma) kuanzia tarehe 23 Februari, 2017. Zoezi la maombi ya udahili lilifungwa rasmi tarehe 06 Machi 2017 ili kuruhusu uteuzi wa kwa waombaji wa kozi hizo.
Baraza linapenda kuwaarifu waombaji wa kozi za Astashahada na Stashahada; na umma kwa ujumla kuwa, matokeo kwa waliochaguliwa kujiunga na vyuo mbalimbali yametangazwa tangu tarehe 25 Machi 2017 kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) uliotumika kufanya maombi ya udahili. Waombaji wanashauriwa kutembelea kurasa zao (profiles) za kuombea udahili kupitia CAS ili kuona kama wamechaguliwa.
Ili kutembelea ukurasa wako, waweza pia kubofya hapa.
BONYEZA HAPA

Imetolewa na
Ofisi ya Katibu Mtendaji
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
Tarehe: 26 Machi, 2017

TAARIFA KUTOKA NACTE KUHUSU KUFUNGULIWA KWA MFUMO WA PAMOJA WA UDAHILI KWA KIPINDI CHA MACHI / APRILI, 2017

BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI
(NACTE)

TAARIFA KWA UMMA

KUFUNGULIWA KWA MFUMO WA PAMOJA WA UDAHILI KWA KIPINDI CHA MACHI/APRILI, 2017 KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017 

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), linapenda kuutangazia Umma na wadau wote wa Elimu nchini, kuwa mfumo wa Udahili wa pamoja yaani “Online Central Admission System (CAS)”, umefunguliwa rasmi tarehe 23 Januari, 2017, saa 6 mchana, kwa kupokea maombi ya mwombaji katika kozi mbalimbali, ikiwemo ngazi ya, Astashahada na Stashahada kwa Kipindi cha Machi/April, 2017 kwa mwaka wa masomo 2016/2017.

Namna ya Kufanya Maombi
Maombi yote yafanyike kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) au kupitia chuoni ambapo mwombaji anapendelea kwenda kusoma, ambapo chuo kitamdahili mwanafunzi husika kwenye mfumo wa udahili kupitia “Institutional Panel”.

Tanbihi: Waombaji wa kozi za Afya waliohitimu Astashahada (NTA Level 5), pia wataomba kwa utaratibu ulioelezwa hapo juu.

Mwombaji wa Astashahada na Stashahada anaweza kuomba kwa ajili ya eneo moja au zaidi katika maeneo ya taaluma yafuatayo:
  1. Biashara, Utalii na Mipango, mfano; Uhasibu, Meneja Rasilimali Watu, Wanyama Pori, Mipango.
  2. Sayansi na Teknolojia Shirikishi, mfano; Kilimo, Uhandisi, Mifumo ya Mawasiliano, Usanifu Majengo, Mifugo.
  3. Afya na Sayansi Shirikishi, mfano; Uganga, Maabara, Ufamasia, Uuguzi.
Sifa za muombaji
  1. Awe amehitimu kidato cha nne mwaka 2015 au kabla ya hapo.
  2. Awe na Astashahada ya mwaka 2016 au kabla ya hapo kwa wanaojiendeleza.
  3. Sifa kwa kozi mahsusi ziko kwenye mwongozo wa kozi (Guidebook) ulioko kwenye mfumo (CAS).
Ada ya maombi ni kama ifuatavyo:
  1. Kwa eneo la Afya na Sayansi Shirikishi ada ya maombi ni Tshs 30,000/=.
  2. Kwa eneo moja kati ya maeneo mengine yaliyobaki, ada ni Tshs 20,000/=.
  3. Kwa zaidi ya eneo moja la taaluma, mfano; Afya pamoja na Biashara, ada ni Tshs 30,000/=, ambapo muombaji anaruhusiwa kuchagua maeneo yote.
Mwisho wa kutuma maombi haya ni tarehe 06/03/2017.
Muhimu: Hakutakuwa na muda wa nyongeza wa kufanya maombi. Hivyo waombaji wanashauriwa kuwa makini wakati wa kufanya maombi yao.


Imetolewa na: 
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

Sunday, 26 March 2017

Breaking News..Rais Magufuli Afanya tena Utenguzi Wizara ya Nishati na Madini


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Joseph Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Prof. Justin Ntalikwa kuanzia leo tarehe 26 Machi 2017.

Katibu Mkuu Ntalikwa aliteuliwa Desemba 2015 na kuapishwa Ikulu Januari 2, 2016.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu, nafasi yake itajazwa hapo baadaye.

Thursday, 23 March 2017

Breaking News!!! Rais Magufuli afanya Mabadiliko baraza la mawaziri, Nape Nauye aondolewa Soma zaidi hapa

Rais Magufuli Leo march 23 Ametengua uteuzi wa Waziri wa Habari, utamaduni na Michezo Mh.Nape Nnauye na nafasi yake kupewa Dkt. Harrison Mwakyembe aliyekuwa Waziri wakatiba na Sheria SOMA HAPA CHINI

Tuesday, 7 March 2017

Gazeti la MwanaHALISI kumuanika Paul Makonda



Screen Shot 2017-03-06 at 09.06.52.png


KILA pembe ya kijiji cha Koromije, Wilaya ya Misungwi, pamoja na viunga vya jiji la Mwanza Paul Makonda, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam anatajwa na kufahamika kama Daudi Albert Bashite, wanaandika Waandishi Wetu.

Wanaomtaja kwa jina hilo ni wanakijiji, ndugu zake, wanafunzi aliowahi kusoma nao pamoja na watu waliowahi kumshuhudia akifanya kazi kama kondakta.

Gazeti la MwanaHALISI baada ya uchunguzi wake wa kina uliohusishwa kutuma timu ya maripota wake jijini Mwanza, wanakuletea habari kamili inayofichua ukweli wa sakata hilo huku mama na baba wa Makonda, shangazi yake na wanafunzi waliowahi kusoma naye wakiwa wamehojiwa.



Shule ya Msingi aliyosoma Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
koromije.jpeg

Chanzo: Mwanahalisi
Makonda 1.JPG
Makonda 2.JPG


 SOURCE ..JF

Sunday, 26 February 2017

Taarifa Muhimu: TCU yatolea ufafanuzi uhakiki wa wanafunzi wasiokuwa na Sifa Vyuoni

Tume ya Vyuo  Vikuu  Tanzania (TCU)  inapenda kuuarifu umma kuwa, uhakiki wa ubora wa wanafunzi wa elimu ya juu

hufanyika kwa mujibu  wa Kifungu  5(1)(b)(c)  cha Sheria ya

Vyuo Vikuu Sura ya 346 ya Sheria za Tanzania.

 

Katika kutekeleza jukumu hili Tume ilianza zoezi la uhakiki kuanzia mwezi Agosti 2016. Hadi kufikia Februari 2017 zoezi

hilo lilikuwa limekamilika kwa vyuo 67 kati ya 84 vinavyotoa shahada ya kwanza. 

Hii ni mara ya kwanza uhakiki wa sifa za wanafunzi wa vyuo  vyote nchini kufanyika kwa wakati mmoja.  Lengo  la uhakiki lilikuwa kujiridhisha kuwa wanafunzi waliopo vyuoni ni wale waliodahiliwa kwa mujibu wa  sheria na taratibu  na kwamba wanakidhi vigezo  stahiki.

 

Uhakiki ulifanyika kwa kulinganisha taarifa za TCU na zile zilizowasilishwa na vyuo.  Uhakiki huo  ulihusisha jumla ya wanafunzi 131,994 waliopo vyuoni kwa mwaka wa masomo 2016/17.

 

Baada ya kulinganisha orodha zilizowasilishwa na vyuo na ile ya TCU ilibainika kuwa wanafunzi 123,827 sawa na asilimia 93.8  wana sifa stahiki.  Aidha jumla ya wanafunzi 8,167 sawa na asilimia 6.2 tu walibainika kuwa na kasoro  katika taarifa za sifa zao.

Kufuatia hali hiyo, Tume ilitoa taarifa kwa umma kuwaomba wanafunzi kurekebisha dosari hizo  kwa kuthibitisha taarifa zao  kupitia vyuo  husika ifikapo  tarehe 28  Februari 2017  ili kuweka kumbukumbu sahihi za mwanafunzi.

 

Hata hivyo  imebainika kuwa taarifa hiyo  imepokelewa kwa mtazamo na hisia tofauti na hivyo kusababisha mkanganyiko vyuoni. Umma unaarifiwa kwamba haikuwa nia wala lengo la Tume kusababisha mkanganyiko huo.

 

Kwa kuwa uhakiki wa sifa za wanafunzi ni kazi endelevu ya Tume na kutokana na maombi ya wadau  mbalimbali,  Tume sasa  itaendelea kuwasiliana moja kwa moja na vyuo  katika kukamilisha zoezi hilo. 

Hivyo  wanafunzi wote waliokuwa wameorodheshwa katika taarifa iliyotolewa awali wanaombwa kuwa watulivu  na kuendelea na masomo  yao kama kawaida.

 

Aidha ifahamike kuwa wanafunzi waliokuwa wameorodheshwa siyo kwamba wamethibitika kuwa hawana sifa stahiki bali kuna dosari katika taarifa zao. Ndiyo sababu Tume iliwaomba kuthibitisha taarifa zao  ili kuondoa dosari hizo.

 

Imetolewa na

Kaimu Katibu Mtendaji

24 Februari 2017

Thursday, 23 February 2017

TCU Yatoa majina ya wanafunzi wa vyuo vikuu ambao hawana sifa ya kuendelea na masomo

Download 
 

Hapa chini ni majina ya wanafunzi wanaoendelea na masomo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambao hawana sifa.

Download

Kuweza kuona majina zaidi ya wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali, bonyeza jina la chuo husika hapa chini kwenye orodha.

Download [45.61 KB]

Thursday, 16 February 2017

Mfumo Mpya wa Kutumia Namba za Simu Kuanzishwa Mwezi Ujao,Utaweza Kuhama Mtandao Mmoja Kwenda Mwingine Bila Kununua Laini Mpya

Mfumo mpya wa matumizi ya namba za simu (Number Portability) unatarajiwa kuanzishwa ifikapo Machi Mosi kwa ushirikiano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kampuni za simu nchini.

Kampuni za simu zilizoingia katika mkataba huo ni pamoja na Tigo, Vodacom, Airtel, TTCL, Zantel, Smile, Smart na Halotel.

Jana, TCRA ilitangaza huduma hiyo mpya kwa watumiaji wa simu nchini, itakayomwezesha mteja kuhama mtandao mmoja kwenda mwingine na kuendelea kutumia namba yake ya awali.

Mpango huo tayari umeshatekelezwa kwenye nchi nyingi za Ulaya na hata Afrika Kusini.

Mmoja wa watumiaji wa mitandao ya simu za mkononi, Musa Aziz amesema pamoja na faida zilizopo bado kuna hofu kwa watumiaji kutokana na usumbufu wa mawasiliano.

“Nafikiri kutakuwa na gharama za ziada mimi nikimpigia mwenzangu sitajua kwa wakati huo anatumia mtandao gani, hapo ninaweza kuingia gharama kubwa zaidi, sina hakika kama italeta unafuu japokuwa ni mpango mzuri,” amesema Aziz.

 

Gallery

Popular Posts

About Us