
New York. Donald John Trump alizaliwa Juni 14, 1946 Jamaica Estates, Queens karibu na New York. Ni mtoto wa pili kati ya watoto watano wa Fred Trump na Mary. Ndugu zake watatu; Maryanne, Elizabeth na Robert wako hai wakati kaka yake mkubwa, Fred Junior alifariki mwaka 1981 kutokana na unywaji pombe wa kupitiliza. Donald anasema jambo hilo ndilo lililomfanya yeye kujiepusha na pombe na uvutaji...