KINGAZI BLOG: 11/09/16

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Wednesday, 9 November 2016

TANZIA:Yule Mtoto Aliyepandikizwa Betri kwenye Moyo Afariki Dunia

Mtoto Happiness Josephat (6) aliyefanyiwa upasuaji wa kupandikiza betri moyoni katika Taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), amefariki dunia. Mama mzazi wa Happiness, Elitruda Malley amesema Happiness alifariki dunia ghafla juzi mchana. Alisema   Jumapili, mtoto huyo alikuwa mzima na walikwenda kanisani kutoa sadaka ya shukrani kama ishara ya kumshukuru Mungu kwa mambo aliyowatendea...

Tahliso yataja makosa ya waombaji wa mikopo

Jumuiya ya wanafunzi taasisi ya Elimu ya Juu,(Tahliso), imesema imebaini kuwa baadhi ya wanafunzi hawakuwasilisha vyeti vinavyohakiki hali zao ikiwamo vyeti vya vifo vya wazazi huku baadhi wakishindwa kuvithibitisha kwa kamishna wa viapo. Hayo yalibainishwa na Mwenyekiti wa Tahliso, Stanslaus Kadugaliza katika taarifa ya Jumuiya hiyo iliyotolewa baada ya kufanyIka kwa kikao cha dharura kilichoshirikisha...

Obama ampongeza Trump, amwalika White House

 Rais Obama amempigia simu Donald Trump kumpongeza kwa ushindi uchaguzi wa urais ambapo pia amemwalika ikulu ya White House mnamo Alhamisi wajadiliane kuhusu shughuli ya mpito. Obama pia amempigia Hillary Clinton na kumpongeza kutokana na alivyofanya kampeni. Rais Obama atatoa taarifa zaidi Jumatano kutoka White House kujadili matokeo ya uchaguzi na hatua ambazo tunaweza kuchukua kama...

Matokeo Marekani 2016: Trump ndiye Rais mteule wa Marekani, amshinda CLINTON majimbo muhimu.

 Wagombea urais wawili wakuu wa urais Marekani Hillary Clinton na Donald Trump wanakaribiana sana katika matokeo ya uchaguzi wa urais katika majimbo muhimu yanayoshindaniwa. Clinton ameshinda Virginia naye Trump akashinda Ohio, Florida, na North Carolina. Kwa sasa Trump ana kura 222 za wajumbe na Clinton 209. Mshindi anahitaji kura 270 za wajumbe. Lakini mgombea wa Republican Bw Trump...

Makonda kupandishwa kizimbani Kisutu leo

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda leo atapanda kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujitetea dhidi ya kesi ya madai ya Sh200 milioni  iliyofunguliwa na waliokuwa makada wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mgana Msindai na John Guninita. Makonda anayetetewa na wakili wa kujitegemea, Seneni Mponda atatoa utetezi wake...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Novemba 9

...
 

Gallery

Popular Posts

About Us