
Mbunge wa Kinondoni, Maulid Mtulia ameliambia Bunge kuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya, Nassib Abdul ‘Diamond Platinumz’, anadaiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) zaidi ya Sh. milioni 400.
Mbunge huyo aliyasema hayo bungeni jana wakati wa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Amesema Wilaya ya Kinondoni ina wasanii wengi maarufu na wamekuwa wakitoa mchango mkubwa...