
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inapenda kuuarifu umma kuwa, uhakiki wa ubora wa wanafunzi wa elimu ya juu
hufanyika kwa mujibu wa Kifungu 5(1)(b)(c) cha Sheria ya
Vyuo Vikuu Sura ya 346 ya Sheria za Tanzania.
Katika kutekeleza jukumu hili Tume ilianza zoezi la uhakiki kuanzia mwezi Agosti 2016. Hadi kufikia Februari 2017 zoezi
hilo lilikuwa limekamilika...