KINGAZI BLOG: 03/24/17

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...

Friday 24 March 2017

VIDEO: Rais Magufuli Katoa ONYO Kwa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Wakati akiwaapisha Dr Harrison Mwakyembe na Prof Palamagamba Kabudi, Ikulu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. John P. Magufuli, leo amewaapisha Dr Harrison Mwakyembe na Prof Palamagamba Kabudi pamoja na mabalozi kadhaa Ikulu Jijini Dar.

Mwakyembe ameapishwa kuwa Waziri mpya wa habari, Profesa Kabudi kaapishwa kaapishwa kuwa waziri wa Katiba na Sheria.

==>Haya ni mambo machache aliyoyasema Rais Magufuli Leo

1.Kuna wengine walisema Kinana leo angezungumza na waandishi, wakati nimemtuma India ambapo atakuwa kwa zaidi ya siku 10

2.Tunataka kuitoa nchi katika hali ya mazoea kuipeleka katika mstari ambao ni sahihi

3.Ukiangalia siku iliyofuata baada ya Rais wa Benki ya Dunia kuja, magazeti yote yaliandika habari nyingine tofauti-

4.Niwatake waandishi wa habari muwe wazalendo, Tanzania ikiharibika na nyie pamoja na wanaowatuma muandike wote mtaharibikiwa

5.Hata magazeti ya leo yana picha ya mtu mmoja ambaye amefanya kosa moja, utadhani kosa ni linaungwa mkono na serikali

6.Niwatake wamiliki wa vyombo vya habari muwe waangalifu, kama mnadhani mna uhuru wa namna hiyo, kuweni makini sana

7.Kuna vyombo vingine vya habari sehemu yenye ugomvi ndio wanapeleka kamera na habari hizo zinapewa muda mrefu, 'watch out'

8.Vyombo vingine haviandiki mazuri ya mtu, lakini wakipata mabaya yake ndiyo yanajaza kurasa

==>Tazama hii Video kumsikiliza Rais Magufuli akiongea Pamoja na walichoongea wateule wa Rais


 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya March 24

Umeipata hii!! Tanzania kuanzisha Kiwanda cha kutengeneza Mabasi.


Balozi wa Hungary hapa nchini mwenye makazi yake Nairobi, Kenya Mhe. Lazaro Eduard Mathe amemhakikishia Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli kuwa nchi yake ipo tayari kushirikiana na Tanzania katika kuendeleza sekta ya viwanda

Pia Balozi huyo amemuhakikishia kwamba wawekezaji kutoka Hungary wameanza kufanya mchakato wa kujenga kiwanda cha kuunda mabasi ya abiria.

Mhe. Lazaro Eduard Mathe amesema hayo leo Ikulu Jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na Mhe. Rais Magufuli muda mfupi baada ya kukabidhi hati zake za utambulisho akiwa ni miongoni mwa Mabalozi sita waliokabidhi hati hizo.

Pamoja na nia ya kujenga kiwanda cha kuunda mabasi ya abiria, Mhe. Lazaro Eduard Mathe amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa juhudi kubwa anazofanya kujenga uchumi wa Tanzania na ameahidi kuwa Hungary itakuza na kuimarisha ushirikiano wake na Tanzania kwa kuleta teknolojia katika sekta mbalimbali ikiwemo viwanda na kilimo pamoja na kuwahimiza wawekezaji kuja kuwekeza nchini Tanzania.

 

Gallery

Popular Posts

About Us