
Mwanamuziki Nay wa Mitego ameachiwa huru kutoka katika Kituo cha Polisi cha Kati Dar es Salaam ikiwa ni saa chache tangu Rais Dkt Magufuli aliporuhusu kuchezwa redioni kwa wimbo wake uliokuwa umefungiwa na BASATA.
Agizo hilo la Rais Magufuli limetolewa leo na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt Mwakyembe alipokuwa akizungumza na waandishi habari mkoani Dodoma.
Waziri Mwakyembe alisema...