
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imeongeza muda wa udahili wa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu mwaka wa masomo 2016/2017 ili kuwapa fursa waombaji ambao wana sifa lakini hawakupata vyuo kutokana na ushindani wa vyuo na kozi walizozichagua.
Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Mtendaji wa TCU Prof. Eleuther Mwageni alipokuwa akiongea na waandishi wa habari juu ya mwenendo mzima wa udahili...