KINGAZI BLOG: KITAIFA

HABARI KARIBU YAKO ZAIDI.

Breaking News
Loading...
Showing posts with label KITAIFA. Show all posts
Showing posts with label KITAIFA. Show all posts

Saturday, 27 May 2017

TLS chini ya Lissu Kama Kweli Wanaitakia Mema Tanzania Waungane Kuzima Wizi wa Acacia

Tumesikia mengi kuhusu Acacia kutuibia Watanzania kwa kutumia mikataba, tena iliyoandaliwa na Watazania wenzetu. Kama taifa, hatuwezi kuendelea kulalamika na kunyoosheana vidole, ni lazima tuchukue hatua. Sheria sio Misahafu. Sheria zimewekwa na binadamu na zinaweza kufutwa au kurekebishwa na binadamu pia.

Pamoja na nguvu ya kifedha waliyonayo Acacia Watanzania wakiungana tutashinda hii vita ya kiuchumi. Sasa, TLS kama kweli wanaitakia mema Tanzania waungane na kusimamia mabadiliko ya sheria ili kufuta vifungu vya kinyonyaji na kuhakikisha kila kinachovunwa kwenye ardhi ya Tanzania kinalipiwa kwa haki, na sio kutumia huu ujanja wa 'commercially viable'.

Ni wazo tu
By Hekima Kwanza

Je Mdau Unaonaje Hapo?

JPM Kutikisa Tena Baraza la Mawaziri..Miongoni mwa Hawa Huenda Akamrithi Prof Muhongo Kwenye Wizara ya Nishati na Madini..!!!


UAMUZI wa Rais John Magufuli kutengua uteuzi wa rafiki yake, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ni wa tatu tangu aunde Serikali, sasa analazimika kukuna kichwa kuteua waziri mwingine kushika nafasi hiyo.

Wakati hilo likisubiriwa, wanasiasa na wasomi wameeleza kuwa hakuna waziri atakayeteuliwa na kusalimika katika wizara hiyo, kwa madai kwamba inazungukwa na rushwa kubwa za kimataifa, mikataba mibovu na kuingiliwa uamuzi na Ikulu.

“Ndiyo maana tumekuwa tukipendekeza kugawanywa kwa wizara hii kwa maana ya kuwa na wizara mbili; ya Nishati na ya Madini,” alisema Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema.

Mei 20 mwaka jana, kwa mara ya kwanza Rais alitengua uteuzi wa rafiki yake mwingine wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga na nafasi yake kuzibwa na Mwigulu Nchemba, ambaye awali alikuwa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, huku Mbunge wa Buchosa, Dk Charles Tizeba akiteuliwa kuchukua mikoba ya Mwigulu.

Mabadiliko ya pili ya Baraza la Mawaziri yalifanyika Machi 23, baada ya mkuu huyo wa nchi kumteua Dk Harrison Mwakyembe kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuchukua nafasi na Nape Nnauye ambaye aliachwa.

Katika mabadiliko hayo, Profesa Palamagamba Kabudi ambaye awali aliteuliwa na Rais kuwa mbunge, alipewa Wizara ya Katiba na Sheria ambayo kabla ya mabadiliko hayo ilikuwa ikiongozwa na Dk Mwakyembe.

Rais hakusubiri Profesa Muhongo ajitathmini, baada ya kupokea taarifa ya uchunguzi wa sakata la kiwango cha madini kwenye kontena, alikiri kuwa na urafiki na Mbunge huyo wa Musoma Vijijini na hilo halikumfanya asite kumwajibisha, kwani baada ya kuisoma ripoti hiyo, Ikulu ilituma taarifa kwa vyombo vya habari ikieleza kuwa Rais ametengua uteuzi wa mtaalamu huyo wa miamba.

Mara zote mbili alizofanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, Rais Magufuli amekuwa na utaratibu wa kuhamisha mawaziri kutoka wizara moja kwenda nyingine au kuteua wabunge na kuwapa wizara.

Katika mabadiliko hayo mawili aliyofanya, ni Dk Tizeba pekee ambaye aliteuliwa kuwa waziri kutoka miongoni mwa wabunge wa majimbo.

Iwapo Rais Magufuli atazingatia utaratibu wa mtangulizi wake Jakaya Kikwete kuteua waziri kutoka mkoa ambao waziri aliyeondoka anatoka, huenda nafasi iliyoachwa wazi na Profesa Muhongo ikajazwa na wabunge kutoka mkoa wa Mara.

Baadhi ya wabunge wa CCM kutoka mkoani Mara ni Boniface Getere (Bunda Vijijini), Nimrod Mkono (Butiama), Vedastus Mathayo (Musoma Mjini), Kangi Lugola (Mwibara) na Lameck Airo (Rorya).

Pia, kauli ya CCM jana kwamba imechoshwa na mauaji yanayotokea kila uchwao mkoani Pwani, ni sawa na kutuma ujumbe kwa Rais Magufuli kwamba kuna tatizo katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuchochea ukubwa wa mabadiliko.

Utaratibu

Miongoni mwa wateule wake ni Naibu Spika, Dk Tulia Ackson. Novemba mwaka 2015 Naibu Mwanasheria Mkuu huyo wa zamani alichukua fomu za kuwania uspika kupitia CCM kabla ya kujitoa dakika za lala salama kisha akateuliwa na Rais Magufuli kuwa mbunge wa viti maalumu.

Baada ya kujitoa, alijitosa kuwania unaibu Spika ambapo wabunge 250 walimpigia kura ya ndiyo.

Wengine walioteuliwa kuwa wabunge na akawapa wizara ni; Waziri wa Mambo ya Nje, Dk Augustino Mahiga, Profesa Makame Mbarawa (Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano), Profesa Joyce Ndalichako (Elimu), Dk Philip Mpango (Fedha) na Dk Abdallah Posi  ambaye alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu.

Hata hivyo, Posi aliteuliwa kuwa balozi kufuatia dosari ya kikatiba katika uteuzi wa wabunge 10 wa kuteuliwa na Rais ambapo Ibara ya 66 (1)(e) inaeleza katika nafasi hizo,  wabunge watano au zaidi wanapaswa kuwa wanawake. Baada ya kuondolewa Posi, Rais alimteua Anne Kilango kuwa Mbunge.

Hivi karibuni, Rais alimteua Salma Kikwete kuwa mbunge na kufanya idadi ya wabunge wanawake wa kuteuliwa na Rais kuwa wanne, kubaki nafasi moja ya uteuzi ambayo ni lazima awe mwanamke.

Mwingine aliyeteuliwa na Rais kuwa mbunge ni Abdlallah Bulembo na kufanya idadi ya wabunge walioteuliwa na kiongozi mkuu huyo wa nchi bila kupewa uwaziri kuwa watatu.

Kwa mantiki hiyo, kama Rais Magufuli atazingatia utaratibu wake wa kuteua mbunge na kumpa wizara, safari hii atalazimika kuteua mbunge mwingine mwanamke.

Iwapo hatateua na kuamua kubadili utaratibu wake, huenda Salma na Kilango wakakumbukwa, huku kukiwa na kila dalili ya baadhi ya mawaziri kuhamishiwa Wizara ya Nishati na Madini.

Wanasiasa, wasomi

Katika maelezo yake, Mbowe alisema madini yanahusisha mafuta, gesi na vito hivyo vikichanganywa na nishati ni mzigo mkubwa.

Alibainisha kuwa wizara hiyo inakabiliwa na vishawishi vingi kutokana na fedha zinazopatikana kwa wawekezaji, jambo ambalo huwa ni mtego kwa mawaziri.

Huku akikosoa mikataba ambayo Serikali imeingia na wawekezaji wa sekta ya nishati na madini, Mbowe alisema ikifuatiliwa kwa undani hakuna atakayebaki salama.

“Yupo Waziri Mkuu mmoja aliondoka kwa kashfa ya wizara hii. Kusema nani atatosha ni ngumu sana kwa wizara hii,” alisisitiza Mbowe.

Mwenyekiti wa Chama Cha Kijamii (CCK), Constatine Akitanda aliitaja wizara hiyo na ya Maliasili na Utalii, kukiri kuwa ni ngumu kuziongoza.

Alidai kuwa mambo mengi yanayoikumba nchi kwa sasa ni matokeo ya nchi kuingia mikataba mibovu, hasa katika utawala wa Serikali ya Awamu ya Tatu.

“Tunachopaswa kufanya ni kuangalia mfumo na mikataba iliyoingiwa. Imetawaliwa na nguvu ya pesa, hakuna waziri atakayekuwa salama,” alisema Akitanda.

Kwa upande wake, kada wa Chadema na mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, David Kafulila alisema:”Madini na nishati ni rasilimali zinazoongozwa kwa rushwa duniani, ni ngumu kutulia.”

Kafulila alisema nchi kadhaa duniani zinapigana kwa sababu ya nishati na madini, jambo alilodai kuwa linaakisi nchini.

Rais wa zamani wa Chama kilichofutwa cha APPT-Maendeleo, Peter Mziray alisema, “Kama Mkapa angeona mbali haya mambo yasingetokea hivi sasa. Alishiriki ubinafsishaji ambao umenufaisha wageni.”

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Dk Frank Tilly alisema kinachoikumba wizara hiyo ni matokeo ya nchi kukosa muundo madhubuti wa uongozi, kusababisha viongozi kufanya mambo wanavyojisikia.

Credit - Jambo Leo

Tuesday, 23 May 2017

MIILI ya Wanafunzi Waliozama Ziwa Victoria Yapatikana ..!!!


Wanafunzi watatu kati ya 24 wa shule ya msingi Butwa,  waliozama katika ziwa Victoria, kisiwa cha Butwa, wamefariki dunia.

 Awali wanafunzi 21 waliokolewa na watatu hawakuonekana lakini saa chache baadaye, miili mitatu iliopolewa. Ajali hiyo ilitokea jana saa 10 alasiri.

 Mkuu wa Wilaya ya  Geita, Herman Kapufi amesema wanafunzi hao walikuwa kwenye mtumbwi waliotumia kuvuka wakitoka shuleni.

MIILI ya Wanafunzi Waliozama Ziwa Victoria Yapatikana ..!!!


Wanafunzi watatu kati ya 24 wa shule ya msingi Butwa,  waliozama katika ziwa Victoria, kisiwa cha Butwa, wamefariki dunia.

 Awali wanafunzi 21 waliokolewa na watatu hawakuonekana lakini saa chache baadaye, miili mitatu iliopolewa. Ajali hiyo ilitokea jana saa 10 alasiri.

 Mkuu wa Wilaya ya  Geita, Herman Kapufi amesema wanafunzi hao walikuwa kwenye mtumbwi waliotumia kuvuka wakitoka shuleni.

Saturday, 20 May 2017

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA WA WATANZANIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA WA WATANZANIA

RAISI WA SERIKALI YA WANAFUNZI ST. JOSEPH AFUKUZWA CHUO KWA KUTETEA HAKI ZA WANAFUNZI WENZAKE

Katika hali ya kusikitisha sana na yenye kuumiza moyo kijana Bachubila Haruna ambae ni Raisi wa serikali ya wanafunzi ya Chuo Cha Mtakatifu Yosefu kampasi ya luguruni amejikuta akipoteza haki yake ya msingi ya kupata elimu katika taifa lake kwasababu ya kutete haki za wanafunzi wenzake.

Mnamo Tarehe 27/03/2017 Raisi Bachubila aliandika barua kwenda Wizara ya Elimu na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) akiomba mrejesho wa serikali kutokana na maagizo aliyoyatoa Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako (mb) kwa uongozi wa chuo na Tume ya Vyuo Vikuu kuhakikisha Elimu na Mazingira ya kusomea Chuoni hapo yanaridhisha wakati wa mgomo wa wanafunzi uliofanyika mapema mwaka jana 2015. Pia Raisi Bachubila alitoa malalamiko ya matatizo mbalimbali na kuomba msaada kutoka ngazi hizo za juu.

Baada ya kuandika Barua hiyo taarifa kupitia mawakala wa Chuo walioko TCU ziliwafikia wahindi ambao ndio wamiliki wa chuo hiko na kwa hali ya kushtukiza walimuandikia Raisi Bachubila barua wakimlaumu kwa kuwasiliana na wizara bila kuwapa taarifa wao, kukichafua chuo nje na kuandika taarifa za uongo.

Baada ya hapo ukapita mda kidogo na kilikuja kukaliwa kikao cha inquiry committee( kamati ya nidhamu ya chuo) kumjadili na kumhoji Raisi Bachubila mnamo tarehe 02/05/2017. Kikao hiko kikatoka na maazimo ya kuishauri seneti ya chuo kupitisha maamuzi ya kumsimamisha chuo mwaka mmoja Raisi Bachubila.

Wakati maamuzi ya seneti yanasubiriwa kukawa kunatokea vuta ni kuvute baina ya wanafunzi na uongozi wa chuo wakitaka kujua nini hatma ya Raisi wao. Wakati huo huo Uongozi wa Chuo kipitia Dean of Students ukawa unamuita Raisi Bachubila ukimlazimisha aandike barua ya kukana barua alioandika kwenda wizarani na ajiuzulu nafasi yake.

Bachubila alikataa kufanya hivo na kubaki na msimamo wake wa kua mtetezi wa wanafunzi wenzake.

Kwa bahati nzuri sana tarehe 16/05/2017 Raisi Bachubila alipokea barua kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge kupitia Katibu mkuu Wizara ya Elimu ikimjibu Raisi Bachubila kua imepokea na ikaipa maagizo Tume ya Vyuo Vikuu kufuatilia malalamiko hayo. Katika hali isiyo ya kawaida Raisi alishangazwa kupokea barua yake ikiwa tayari imeshafunguliwa na inaonyesha kucheleweshwa kupewa maana barua hiyo Ofisi ya Waziri Mkuu iliijibu tarehe 08/05/2017.

Baada ya barua hiyo kuja siku iliyofuata tarehe 17/05/2017 Chuo kilimuandikia Rasmi Raisi Bachubila kua kimemfukuza chuo kupitia Principal wa chuo.

Wanafunzi wengi hatujafurahishwa na hatua hii na tunaipinga vikali. Kwani ni uonevu wa wazi kwa mtetezi wetu. Msimamo wake juu ya maslahi yetu ya Elimu ndio umesababisha leo hii amefukuzwa chuo. Hivo sisi kama wanafunzi tuko tayari kufanya lolote hata kama ni kuacha shughuli za kitaaluma mpaka pale mwenzetu, kaka yetu na kiongozi huyu atakapo rudishwa masomoni kwa nafasi yake ile ile ya Uraisi.

Mbali na hapo serikali iyopita ya wanafunzi ilikua ikiwasiliana na wizara na TCU hadi kufanikiwa kumleta Waziri wa Elimu Profesa Ndalichako hapa chuoni ila hata siku moja haikuwahi kukipa chuo Taarifa yoyote na hamna kiongozi yoyote wa serikali zilizopita aliewahi kufukuzwa chuo kwasababu ya kudai haki katika mamlaka husika.

Ni ukweli kusema kwamba Chuo hiki cha St. Joseph ndugu watanzania wenzetu kimegubikwa na uchafu na wizi mkubwa wa kitaaluma na fedha za watanzania. Hapa chuoni tunalipa ada kubwa TSH 3000000/= na tunalazmishwa kuilipa yote kwa mkupuo lakini cha kushangaza katika idara mbalimbali wameajiri walimu wakihindi ambao hata elimu ya kuweza kufundisha Chuo Kikuu hawana ila tunalazmishiwa hivo hivo wakati hata lugha ya kufundishia ambayo ni kingereza hawajui.

Chuoni kwetu mitihani imekua ikisahishwa ovyo ili kuwapa wanafunzi Suplementary nyingi. Hatukatai kua hata katika vyuo vingine vya uhandisi Supp hutolewa kwa wingi ila tofauti ni kua wenzetu hao hua hawalipii Supp ila sisi tunalipia Supp shilingi 10000/= kwa somo moja. Hivo uongozi wa chuo umefanya kama mtaji wa kupata kipato cha ghafla.

Ikumbukwe kua Chuo hiki kilinyimwa intake ya wanafunzi wapya wa mwaka wa kwanza mwaka uliopita huku wizara ikikipa mda wa kujifanyia marekebisho ili kipate intake mwaka huu, ila cha kushangaza chuo kimeendelea na utaratibu mbovu usiokidhi.

Tunawaomba watanzania kwa ujumla, Viongozi wa nchi na Wizara pamoja na TCU waliangalie hili kwa jicho la tatu maana kama chuo hiki kitaendelea kutoa wahandisi feki basi ni hatari mno kwa maendekeo ya taifa letu.

Tunawaomba wadau mbalimbali wa Elimu nchini na wapenda haki kuingilia kati swala hili maana sisi wanafunzi na uongozi wa chuo inaonekana hatuwezi kufikia muafaka bora. Wanahabari mtusaidie kutangaza hili ili jamii ijue kiundani kinachoendelea St. Joseph.

Tchaooo
IMG-20170520-WA0013.jpg

BASHITE Avutiwa Pumzi...Hbari Vichwa vya Magazeti y Leo Jumamosi 20/5/2017.



UTATA Waibuka Wakili Aliyefia Sebuleni Dar..Maiti Yake Yakutwa na Damu Kichwani.


WAKILI wa kujitegemea, Noel Ndalu, amekutwa amefariki sebuleni nyumbani kwake Sinza jijini Dar es salaam, kifo ambacho kimeacha maswali kadhaa kutokana na mazingira yake.

Jana, Nipashe ilifika nyumbani kwa wakili huyo aliyekuwa akiishi Sinza kwa Remmy wilayani Kinondoni na kupata simulizi zenye kuibua maswali juu ya kifo hicho.

Baadhi ya maswali hayo ni pamoja na sababu za kifo chake kilichoonekena kuwa cha ghafla, hasa kwa kutambua kuwa kazi zake huhusisha kesi zitokanazo na masuala mbalimbali ya migogoro ya kisheria wanayokumbana nayo wateja wake.

“Inasikitisha sana…kifo chake ni cha ghafla na kwakweli hatujui ni kitu gani kimemkuta…labda alikuwa akisumbuliwa na maradhi kama ya kifafa ambayo wakati mwingine huwafanya watu wanaoishi peke yao wapoteze maisha kwa namna hii. Hakuna anayejua kwakweli,” mmoja wa majirani aliiambia Nipashe kuhusiana na taarifa za kifo cha wakili huyo.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Suzan Kaganda, hakuweza kuzungumzia tukio hilo jana baada ya kueleza kuwa ametingwa na kikao, lakini baadhi ya majirani wameeleza kushangazwa na kile kilichomtokea mwenzao huyo.

Akizungumza na Nipashe, mama mwenye nyumba aliyokuwa amepanga wakili huyo, iliyopo katika Mtaa wa Mtendaji, Salama Shaaban (50), alisema Wakili Noel alikutwa amefariki sebuleni kwake juzi majira ya saa 4:00 asubuhi.

Alisema mara ya mwisho kuonana na mpangaji wake huyo ilikuwa ni Jumanne, saa 12:00 jioni wakati wakili huyo akimkabidhi stakabadhi ya uniti za umeme wa Luku aliokuwa amenunua.

“Jumanne alikuja hapa akaniambia mama nimekuletea umeme, nikamwambia ahsante mwanangu na alikuwa ni mzima wa afya...na tangu siku hiyo nikawa sijamuona kwa sababu anaishi upande wa pili wa nyumba yangu na ana geti lake,” alisema Salama.

Alieleza kuwa, hawakuwa na kawaida ya kuonana mara kwa mara na ndiyo sababu hakushtuka kutomuona kwa siku zote hizo.

“Hapa wako wapangaji wawili, marehemu na mwingine. Sasa jana asubuhi, nikiwa ndani kwangu, alikuja mpangaji mwenzake, akaniambia mama simu inaita muda mrefu ndani kwa Noel na hakuna anayepokea na yeye hajamuona akitoka,” alisema.

Alisema baada ya kupewa taarifa hizo, alitoka yeye na kijana wake kwenda hadi kwenye mlango mkubwa wa wakili Noel na kuanza kugonga. Walifanya hivyo kwa muda mrefu bila majibu na ndipo nao wakingiwa na wasiwasi.

“Chini ya mlango kuna uwazi hivyo mwanangu aliamua kuchungulia, akaniambia mama sioni kitu lakini nasikia harufu ya kitu kilichooza inatoka ndani,” alisema Salama.

Alisema mtoto wake huyo alichukua fimbo ndefu na kuipitisha chini ya mlango ambao upo karibu na dirisha kwa ajili ya kusukuma pazia ili waweze kuchungulia dirishani.

“Tulifanikiwa kusogeza pazia na tukachungulia ndani… tukamuona Noel akiwa amelala chali chini ya sakafu kuelekea mlango wa chumbani na kwenye paji lake la uso kulikuwa na damu zimechuruzikia kwa chini,” alisema.

Alisema baada ya kuona hali hiyo, waliamua kwenda kuwaita wajumbe wa mtaa wao ambao walifika na kushuhudia tukio lile kabla ya kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi Mabatini.

“Baadaye Polisi walikuja na gari. Waliamuru mlango uvunjwe, wakaingia ndani na kuuchunguza mwili. Wakakuta amechanika kwenye paji la uso wake,” alisimulia Mama Salama.

Alisema pia alikutwa amevaa kaptura na hawakukuta silaha ya aina yoyote. Baada ya hapo polisi waliuchukua mwili huo na kwenda kuuhifadhi katika Hospitali ya Mwananyala.

Akisimulia namna anavyomfahamu, Salama alisema wakili huyo binafsi ambaye alikuwa na ofisi yake Temeke jijini Dar es Salaam, ameishi kwenye nyumba yake kwa miaka mitatu.

Alisema awali alikuwa akiishi na mwanamke ambaye aliondoka miaka miwili iliyopita, na hivyo hadi umauti ukimkuta alikuwa akiishi peke yake.

“Mke wake aliondoka na mtoto wa miezi miwili. Kwa hiyo alikuwa akiishi peke yake,” alisema Salama.

Alisema baada ya kifo hicho, mjomba wake alifungasha mali za wakili huyo na kuondoka nazo na kwamba jana, waliuaga mwili wake katika Hospitali ya Mwananyamala na kusafirisha kwenda Dodoma kwa maziko.

“Baba yake anaishi Dodoma hivyo leo (jana) walienda Mwananyamala saa 4:00 kwa ajili ya kuuchukua mwili kuusafirisha,” alisema.

MAWAKILI WAMLILIA

Aidha, Chama cha Wanasheria Tanganyika(TLC), kilitoa taarifa ya kifo cha aliyekuwa mwanachama wao mwenye namba ya usajili 4644, Noel Ndalu .

Taarifa iliyotolewa na uongozi wa TLC kwa wanachama wake, ilieleza kuwa, mwanachama huyo alifariki Jumanne ya wiki hii, Mei 16 na kwamba aliagwa jana katika Kanisa la Kaloloni Chang’ombe na baadae kusafirishwa kuelekea mkoani Dodoma kwa maziko

POLISI Waua Majambazi Matatu Katika Vita ya Majibizano ya Risasi Iliyoshangaza Watu Mwanza..!!

WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wameuawa kwa risasi jijini Mwanza jana katika kile kinachoelezwa kuwa ni matokeo ya vita kali ya kurushiana risasi baina ya watuhumiwa hao na askari wa Jeshi la Polisi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, alisema tukio hilo limetokea katika eneo la viwanja vya ST. Mary’s Mtaa wa Ndofe wilaya ya Nyamagana, ambako polisi walikuwa wameweka mtego baada ya kupata taarifa kuwa watuhumiwa walipanga kufanya uhalifu.

Ilielezwa zaidi kuwa polisi waliwafikia watuhumiwa baada ya kumkamata mganga wa kienyeji aitwaye Ayubu Nyamweru (45), mkazi wa Katoro mkoani Geita, ambaye alikutwa akiwa na kompyuta mpakato tatu na simu moja aina ya Sumsung vilivyokuwa imeibwa katika tukio la kuvunja nyumba maeneo ya Nyamanoro.

Tukio la kuporwa kwa vitu hivyo lilihusisha pia kuporwa kwa bastola aina ya Duty CZ 75P-07 na fedha, siku ya Mei 13 mwaka huu na kufunguliwa jalada lenye namba NY/IR/3773/2017.


Ilielezwa na polisi kuwa baada ya mganga Nyamweru kuhojiwa, alitaja wenzake anaoshirikiana nao katika kufanya matukio mbalimbali ya uvunjaji na unyanga’anyi jijini Mwanza na maeneo ya jirani.

Ilielezwa kuwa kufuatia maelezo ya mganga huyo, ndipo polisi walipofuatilia na kumkamata mtuhumiwa mwingine (Benedicto Thobias) kabla ya kuweka mtego uliosababisha kutokea kwa majibizano ya risasi baina yao na majambazi hao.

Akizungumza jana, Kamanda Msangi aliwataja watuhumiwa wlaiofariki kwa kupigwa risasi katika mapambano hayo kuwa ni Benedicto Thobias ambaye ni mkazi wa Nyamatara Buhongwa na wengine waishio pia Mwanza ni Mabula Segeja na Charles Thomas.

 “Mnamo Mei 19 mwaka huu, katika viwanja vya ST. Mary’s mtaa wa Ndofe wilaya ya Nyamagana walifika watu watano ambao walikuwa ni wenzake na mtuhumiwa Benedicto. Askari walipowaamuru wajisalimishe walikaidi amri hiyo na kuanza kufyatua risasi uelekeo wa askari,” alisema Msangi na kuongeza:

“Ndipo askari wakajibu mapigo na kuwajeruhi majambazi wawili na zile risasi walizozipiga ziliweza kumjeruhi mwenzao (Benedicto) aliyekuwa amewapeleka askari kwenye eneo lile… wote watatu walifariki dunia wakati wanapelekwa hospitali kwa matibabu.”

Aidha, Kamanda Msangi alisema kuwa katika tukio hilo, polisi walifanikiwa kukamata silaha mbili ambazo ni bastola aina ya Duty CZ 75P -07 yenye namba B.512637 ikiwa na risasi 15 na magazini mbili na short gun iliyofutika namba ikiwa na risasi mbili na maganda mawili ya risasi, mali ya Suleimani Waziri aliyekuwa akiimiliki kihalali.

Kwa mujibu wa Kamanda Msangi, miili ya watuhumiwa hao imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa ajili ya uchunguzi na utambuzi zaidi wakati msako wa kuwasaka wenzao waliotoroka na wengine waliokuwa wakishirikiana nao bado ukiendelea.

Credit - Nipashe

UTATA Waibuka Wakili Aliyefia Sebuleni Dar..Maiti Yake Yakutwa na Damu Kichwani.


WAKILI wa kujitegemea, Noel Ndalu, amekutwa amefariki sebuleni nyumbani kwake Sinza jijini Dar es salaam, kifo ambacho kimeacha maswali kadhaa kutokana na mazingira yake.

Jana, Nipashe ilifika nyumbani kwa wakili huyo aliyekuwa akiishi Sinza kwa Remmy wilayani Kinondoni na kupata simulizi zenye kuibua maswali juu ya kifo hicho.

Baadhi ya maswali hayo ni pamoja na sababu za kifo chake kilichoonekena kuwa cha ghafla, hasa kwa kutambua kuwa kazi zake huhusisha kesi zitokanazo na masuala mbalimbali ya migogoro ya kisheria wanayokumbana nayo wateja wake.

“Inasikitisha sana…kifo chake ni cha ghafla na kwakweli hatujui ni kitu gani kimemkuta…labda alikuwa akisumbuliwa na maradhi kama ya kifafa ambayo wakati mwingine huwafanya watu wanaoishi peke yao wapoteze maisha kwa namna hii. Hakuna anayejua kwakweli,” mmoja wa majirani aliiambia Nipashe kuhusiana na taarifa za kifo cha wakili huyo.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Suzan Kaganda, hakuweza kuzungumzia tukio hilo jana baada ya kueleza kuwa ametingwa na kikao, lakini baadhi ya majirani wameeleza kushangazwa na kile kilichomtokea mwenzao huyo.

Akizungumza na Nipashe, mama mwenye nyumba aliyokuwa amepanga wakili huyo, iliyopo katika Mtaa wa Mtendaji, Salama Shaaban (50), alisema Wakili Noel alikutwa amefariki sebuleni kwake juzi majira ya saa 4:00 asubuhi.

Alisema mara ya mwisho kuonana na mpangaji wake huyo ilikuwa ni Jumanne, saa 12:00 jioni wakati wakili huyo akimkabidhi stakabadhi ya uniti za umeme wa Luku aliokuwa amenunua.

“Jumanne alikuja hapa akaniambia mama nimekuletea umeme, nikamwambia ahsante mwanangu na alikuwa ni mzima wa afya...na tangu siku hiyo nikawa sijamuona kwa sababu anaishi upande wa pili wa nyumba yangu na ana geti lake,” alisema Salama.

Alieleza kuwa, hawakuwa na kawaida ya kuonana mara kwa mara na ndiyo sababu hakushtuka kutomuona kwa siku zote hizo.

“Hapa wako wapangaji wawili, marehemu na mwingine. Sasa jana asubuhi, nikiwa ndani kwangu, alikuja mpangaji mwenzake, akaniambia mama simu inaita muda mrefu ndani kwa Noel na hakuna anayepokea na yeye hajamuona akitoka,” alisema.

Alisema baada ya kupewa taarifa hizo, alitoka yeye na kijana wake kwenda hadi kwenye mlango mkubwa wa wakili Noel na kuanza kugonga. Walifanya hivyo kwa muda mrefu bila majibu na ndipo nao wakingiwa na wasiwasi.

“Chini ya mlango kuna uwazi hivyo mwanangu aliamua kuchungulia, akaniambia mama sioni kitu lakini nasikia harufu ya kitu kilichooza inatoka ndani,” alisema Salama.

Alisema mtoto wake huyo alichukua fimbo ndefu na kuipitisha chini ya mlango ambao upo karibu na dirisha kwa ajili ya kusukuma pazia ili waweze kuchungulia dirishani.

“Tulifanikiwa kusogeza pazia na tukachungulia ndani… tukamuona Noel akiwa amelala chali chini ya sakafu kuelekea mlango wa chumbani na kwenye paji lake la uso kulikuwa na damu zimechuruzikia kwa chini,” alisema.

Alisema baada ya kuona hali hiyo, waliamua kwenda kuwaita wajumbe wa mtaa wao ambao walifika na kushuhudia tukio lile kabla ya kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi Mabatini.

“Baadaye Polisi walikuja na gari. Waliamuru mlango uvunjwe, wakaingia ndani na kuuchunguza mwili. Wakakuta amechanika kwenye paji la uso wake,” alisimulia Mama Salama.

Alisema pia alikutwa amevaa kaptura na hawakukuta silaha ya aina yoyote. Baada ya hapo polisi waliuchukua mwili huo na kwenda kuuhifadhi katika Hospitali ya Mwananyala.

Akisimulia namna anavyomfahamu, Salama alisema wakili huyo binafsi ambaye alikuwa na ofisi yake Temeke jijini Dar es Salaam, ameishi kwenye nyumba yake kwa miaka mitatu.

Alisema awali alikuwa akiishi na mwanamke ambaye aliondoka miaka miwili iliyopita, na hivyo hadi umauti ukimkuta alikuwa akiishi peke yake.

“Mke wake aliondoka na mtoto wa miezi miwili. Kwa hiyo alikuwa akiishi peke yake,” alisema Salama.

Alisema baada ya kifo hicho, mjomba wake alifungasha mali za wakili huyo na kuondoka nazo na kwamba jana, waliuaga mwili wake katika Hospitali ya Mwananyamala na kusafirisha kwenda Dodoma kwa maziko.

“Baba yake anaishi Dodoma hivyo leo (jana) walienda Mwananyamala saa 4:00 kwa ajili ya kuuchukua mwili kuusafirisha,” alisema.

MAWAKILI WAMLILIA

Aidha, Chama cha Wanasheria Tanganyika(TLC), kilitoa taarifa ya kifo cha aliyekuwa mwanachama wao mwenye namba ya usajili 4644, Noel Ndalu .

Taarifa iliyotolewa na uongozi wa TLC kwa wanachama wake, ilieleza kuwa, mwanachama huyo alifariki Jumanne ya wiki hii, Mei 16 na kwamba aliagwa jana katika Kanisa la Kaloloni Chang’ombe na baadae kusafirishwa kuelekea mkoani Dodoma kwa maziko

Friday, 19 May 2017

Kutana na Mama aliyejifanya mwanaume ili afanye kazi mgodini Tanzania

Pili Hussein alitamani kujiimarisha kimaisha na mawe ya thamani yanayosemekana kuwa nadra mara elfu mia moja kuliko almasi, lakini kwa kuwa wanawake hawakuwa wanaruhusiwa kwenye migodi hiyo alivalia mavazi kama mwanamume na kuwadanganya wafanyikazi wenzake kwa zaidi ya mwongo mmoja.

Pili alilelewa katika familia kubwa mjini Tanzania. Mtoto wa mchugaji ambaye aliyekuwa na mashamba makubwa, babake Pili alikuwa na wake sita na alikuwa miongoni mwa watoto 38.

Licha ya hayo yote alilelewa vyema kwa njia tofauti.

''Babangu alinichukulia kama mwanamume na nilikuwa nikichunga mifugo yake, lakini sikuyapenda maisha hayo kabisa'', alisema.

Hata ndoa yake haikuwa ya furaha, akiwa na umri wa miaka 31 Pili aliikimbia ndoa yake iliyokumbwa na migogoro ya kinyumbani.

Alipokuwa akitafuta ajira alijipata katika mji mdogo wa Mererani, Tanzania, uliopo chini ya mlima mkuu wa Kilimanjaro.

Eneo hilo ni maarufu sana duniani kwa kuwa na madini nadra ya rangi ya samawati ya tanzanite.

''Sikwenda shule , kwa hivyo sikuwa na mambo mechi kuchagua,'' Pili alisema.

''Wanawake wahakuruhusiwa kwenye maeneo ya migodi hiyo, nikajitosa kama mwanamume shupavu na mwenye nguvu. Nilichukua suruali ndefu na kuzikata zikawa kama kaputula ili kufanana na mwanamume. Hivyo ndivyo nilivyofanya.''

Ili kukamilisha mabadiliko yake , alibadilisha pia jina lake.

''Niliitwa Uncle Hussein {akimaanisha mjomba Hussein}, sikumwambia yoyote kuhusiana na jina langu halisi la Pili.

Hata leo ukija katika kambi hiyo utanitafuta kwa jina hilo la Uncle Hussein.''

Kwenye migodi hiyo yenye joto ,uchafu mwingi na wenye kina cha mita mia moja chini ya ardhi Pili angefanya kazi kwa saa 10-12 kwa siku , akilima na kuchunga akiwa na matumaini ya kupata mawe hayo ya thamani kwenye mishipa ya mawe hayo ya grafiti.

''Ningeenda hadi mita 600 chini ya mgodi, mara kwa mara nikiwa shupavu kuliko wanaume wengine.

Nilikuwa na nguvu nyingi na niliweza kufanya kazi kama matarajio ya wanaume wengine wangefanya.''

Pili amesema hakuna aliyemshuku alikuwa mwanamke.

''Nilijifanya kama nyani aina ya Gorilla'' alisema, Nilipigana, lugha yangu ilikuwa mbaya , nilibeba kisu kikubwa kama Maasai.

Hakuna mtu alifahamu kwamba mimi ni mwanamke kwa sababu kile nilichokuwa nikifanya nilikifanya kama mwanamume.''

Baada ya mwaka mmoja, alipata utajiri , alipopata mawe mawili makubwa ya Tanzanite. Kutokana na pesa alizozipata alimjengea babake, mama na pacha wake nyumba mpya na akajinunulia vifaa zaidi na akaanza kuajiri wachimba migodi kumfanyia kazi.

Na kujificha kwake kuliwashawishi kwamba alichukua hatua zisizo za kawaida kwa utambulisho wake kujulikana.

Mwanamke mmoja aliripoti kwamba alikuwa amebakwa na wachimba migodi Pili akiwa miongoni mwa washukiwa.

''Polisi walipokuja, wanaume waliotekeleza ubakaji huo wakasema: 'Huyu ndio mwanamume aliyetekeleza hilo'' na nilipopelekwa katika kituo cha polisi , Pili akasema alikuwa hana namna bali kutoboa siri yake.''

''Aliwauliza polisi kumleta polisi mwanamke ili amchunguze kwamba yeye hakutekeleza kitendo hicho na baadaye aliachiliwa huru. Hata baada ya hilo wachimba migodi wenzake waliona vigumu kuamini walikuwa wamedanganyika kwa siku nyingi''.

''Hawakuamini hata polisi waliposema kwamba alikuwa mwanamke," alisema, ''haikuwa rahisi kwao kukubali hadi mwaka 2001 nilipoolewa na nikaanza familia.''

Kutafuta bwana wakati kila mtu amenizoea kama mwanamume haikuwa rahisi, Pili alipata bwana na akafanikiwa.

Swali lililokuwa akilini mwake lilikuwa,'je ni mwanamke kweli?'' anakumbuka. ''ilimchukua miaka mitano ndipo aliponikaribia.''

Pili aliikuza taaluma yake na hivi leo anamiliki kampuni yake ya migodi ambayo ameajiri wachimba migodi 70 , watatu kati yao ni wanawake, lakini wanafanya kazi ya upishi.

Pili amesema licha ya kwamba kuna wanawake wengi katika makampuni ya migodi kuliko wakati wake, hata leo ni wanawake wachache wanaofanya kazi kwenye migodi hiyo.

''Wanawake wengine huyaosha mawe hayo , wengine ni wakala na wengine ni wapishi'' , alisema, ''lakini hawaingii ndani ya migodi , si rahisi kumpata mwanamke akifanya nilichofanya wakati wangu.''

Mafanikio ya pili yamemuezesha kuwalipia karo watoto wa ndungu zake 30 na wajukuu. Licha ya hayo amesema hawezi kumrai mwanawe kufuata nyayo zake.

''Najivunia kwa kile nilichokifanya, imenifanya tajiri lakini ilikuwa vigumu kwangu'', amesema.

''Nataka kuhakikisha mtoto wangu ataenda shule apate elimu na ataweza kujiendeleza kimaisha kwa njia tofauti mbali na nilivyopitia.''

MRISHO Gambo: Serikali Itaendelea Kuwadhibiti Wote Watakaotaka Kuingiza Siasa Kwenye Majanga


Serikali mkoani Arusha imewataka wananchi na taasisi zinazoendelea kutoa rambirambi kwa familia za wanafunzi waliofariki katika ajali ya basi la wanafunzi kufuata taratibu zilizowekwa ili kuepusha migongano isiyo ya lazima. Aidha amesema serikali itaendelea kuwadhibiti wote watakaotaka kuingiza siasa kwenye majanga likiwemo la vifo vya wanafunzi na amesisitiza umuhimu wa kila mmoja kufuata sheria taratibu na maelekezo yanayotolewa na serikali.

Nape Nnauye afunguka kuhusu ukimya wa Kinana, Mwenendo wa shughuli za Bunge pamoja Polisi Kutumia Nguvu Kubwa

Na Regina Mkonde 

 Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye amefunguka kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo, ukimya wa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, muenendo wa shughuli za Bunge pamoja na tukio lililotokea hivi karibuni la Askari Polisi mmoja wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kufyatua risasi hewani mbele ya aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima baada ya kutokea majibizano yaliyosababishwa na dereva wa Malima kuegesha gari vibaya.

Nape amefunguka hayo jana  jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na wanahabari ambapo alisema, Kinana ambaye baadhi ya watu wanadai kuwa ukimya wake umetokana na kujiuzulu, yuko katika wadhifa wake wa ukatibu mkuu na anaendelea kufanya kazi za chama.

“Mimi sio msemaji wa chama, lakini Katibu Mkuu yupo na anafanya kazi yake kama kawaida…., mimi bado ni mwanachama na muumini mzuri wa CCM inayopenda haki, na nina amini hiki ndicho chama pekee bora kitakachoweza kuwakomboa watanzania pamoja na kuamiwa ikiwa kitatekeleza mkataba wake na wananchi ambao ni wa kutimiza ahadi zake ilizo ziahidi,” alisema.

Kuhusu tukio la Askari Polisi kufyatua risasi hewani, ambalo Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamanda Simon Sirro alisema ulikuwa uamuzi wa busara wa kuondoa taharuki katika tukio hilo, na mbinu ya kuwatia nguvuni watuhumiwa.

Nape alishauri vyombo vya dola kutotumia nguvu kwani kitendo hicho kitajenga hofu na chuki baina ya serikali na wananchi na hata kwa chama tawala CCM, huku akiisihi serikali kuondoa vitendo vinavyotia hofu wananchi.

“Ni vizuri vyombo vya dola vikatimiza majukumu yake kwa kuwa ni vyombo vya wananchi, si vizuri vikitumia nguvu kubwa pale isipostahili. Ifikie hatua raia asiye na silaha Polisi wasitumie nguvu kushughulika naye kwa kutumia silaha. Nimeona ile video ikionyesha Malima alikuwa anauliza chanzo cha tatizo,”alisema na kuongeza.

“Kuna nchi tamaduni zake ni kutumia mabavu na nyingine zinatumia demokrasia, nchi yetu utamaduni wake si wa kutumia nguvu, tumezoea kuelewana kwa mazungumzo. Vyombo vya dola visitumie nguvu kwa kuwa tunajenga usugu usio na maana. Na kama kuna mazingira hatarishi basi nguvu itumike.”

Kuhusu mienendo ya shughuli za Wabunge Bungeni, aliwataka wabunge kutekeleza majukumu yao ikiwemo kuwawakilisha na kusimamia vema masilahi ya wananchi wanaowawakilisha, pamoja na kuisimamia serikali kutekeleza vizuri majukumu yake.

“Bunge ni mkutano wa wananchi, na wabunge wapo kwa niaba ya wananchi katika kupitisha na kushauri mipango ya serikali. Ni vizuri wasimame katika maeneo yao, wasiwe wapiga makofi, pale serikali inapofanya vizuri ipongezwe na inapofanya vibaya ikosolewe,” alisema.

Kuhusu Uhuru wa Vyombo vya Habari, alisema ifikie hatua wananasiasa wawe na ngozi ngumu ya kuvumilia kukosolewa  na watu kupitia vyombo vya habari. Pia ameshauri wananchi wanaotaka maonesho ya vikao vya bunge moja kwa moja, kuuomba mhimili huo kubadilisha sheria zake ambazo zimeipa mamlaka ya kuamua namna ya kuendesha shughuli zake.

“Naamini uamuzi wa siku ile wa kuzuia shughuli za bunge live ulikuwa sahihi sababu sheria zinasema Bunge litaendeshwa kwa sheria zake. Wananchi wanaozungumzia Bunge live, waliombe libadilishe sheria zake ili lianze kuonyeshwa live,” alisema


Friday, 12 May 2017

Ofisi ya Rais yakanusha taarifa inayosambazwa mitandaoni kuhusu vigezo vya utoaji ajira



Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma afariki dunia leo

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu amefariki dunia leo saa nne asubuhi katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)

Mdogo wa marehemu, Shaibu Mwambungu amesema kaka yake alifariki dunia leo asubuhi baada ya hali yake kubadilika ghafla akiwa hospitalini hapo.

Shaib amesema taratibu za mazishi zitatolewa baadaye ambapo kwa sasa anajiandaa kusafiri kutoka Songea kuja jijini Dar es salam kwa ajili ya mazishi.


TUHUMA za Mateso Dhidi ya Wafanyakazi wa Ndani Oman, Mtanzania Afunguka Makubwa


Wafanyakazi wa majumbani walioko Oman wanatoka kila mahala duniani. Wafilipino peke yao ni wengi mara nyingi sana kuliko Watanzania na huwasikii ila wachache sana kulalamika. Lakini idadi ya walalamikaji kutoka Tanzania ndiyo iliyo kubwa kabisa ingawa jumla yao ni ndogo sana Oman.

Wapendwa waungwana na wapenda ukweli. Siku hizi za karibuni kumekuwako na upotoshwaji mkubwa wa habari za wafanyakazi wa ndani nchini Oman. Jamani waungwana, Waswahili husema kunya anye kuku akinya bata huambiwa kaharisha. Hizo habari za mayaya Oman ni za fitina na uchochezi uliokithiri na hazitamsaidia mtu yoyote, maana sisi ndio wahitaji zaidi wa hizo ajira nje ya nchi yetu.

Nchi za GCC zimekuwa na utaratibu wa miaka mingi kuajiri wafanyakazi kutoka nchi za Asia. Kwa kuzingatia msemo “mfae nduguyo kwanza” ndipo Waomani wakawa pia na utaratibu wa kuwaajiri wafanyakazi kutoka Afrika Mashariki, kwa kuwa kuna historia ya muda mrefu na ya kidugu baina yao. Sasa imekuwa balaa kila kukicha ni matusi yasiyokuwa na maana ila kutapakaza fitina na chuki kwenye mitandao ya kijamii na hata baadhi ya vyombo vya habari kama vile magazeti na televisheni.

Bora nitangulize kusema kitu kimoja ambacho mtu yeyote mwenye akili zake timamu na kupenda kusikia ukweli hawezi kukikataa, nacho ni kuwa hakuna nchi yoyote duniani ambayo haina watu wema na pia watu waovu. Mambo ni kuzidiana tu. Wala hakuna nchi yenye matajiri wenye kuajiri wafanya kazi pasitokee wenye kudhulumu na wenye kudhulumiwa. Kwa vile nazijua vizuri nchi mbili hizi — Tanzania na Oman — naweza pia kusema kwa uhakika kuwa baina ya Tanzania na Oman, utakuta kuwa dhulma wanazotendewa wafanyakazi wa majumbani Tanzania ni kubwa zaidi ukilinganisha na Oman.

Hapa Tanzania wapo wafanyakazi wanaoteseka kila siku na jamaa zao wenyewe kwa mshahara wa shilingi 20,000 au 40,000 kwa mwezi. Sio hilo tu la mshahara, bali hata siku za mapumziko za Jumamosi na Jumapili au zile sikukuu za kitaifa, hawapewi. Haya ni ya ukweli kabisa na wala sio siri. Ukitaka kumtoa mtu kijiti jichoni mwake, kwanza jiangalie kama jicho lako halina boriti.

Hapa Tanzania wafanyakazi wana kila mateso lakini wanavumilia tu. Ukifuatilia kwa makini utagundua kuwa haya ya uchochezi uliojaa fitina unatokana na kundi fulani ambalo hawapendelei pawe na masikilizano mema baina ya Waarabu na Waafrika. Na lengo lao hasa hata si Waarabu. Ukipeleleza kwa makini utagundua kuwa wanachokichukia kweli ni dini waliyoileta Waarabu, nayo ni Uislamu.

Katika siku za hivi karibuni kuna sauti zinatumwa na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii, hasa WhatsApp na Instagram, zikidai kuwa kuna wafanyakazi wa majumbani nchini Oman wanateswa vibaya hadi kusema kuwa wanauawa kwa makusudi na wengine wanapangiwa njama za kuuliwa ili wawe mihanga kwa majini ya Kiomani. Mojawapo ni sauti ya mama mtu mzima ambaye dhahiri kabisa inaonekana kuwa alitumwa kusudi kutukana dini ya Kiislamu.

Hilo ndilo lengo lao hasa, maana hakuwa na haja ya kutaja maneno kama vile kuwa watu wanasali sala tano kila siku halafu wanatesa watu. Hiyo haikuhusu kabisa. Ikiwa sala tano zinawaudhi basi wataumia sana. Mimi binafsi nimeishi na Mlokole wa Kanisa la Efatah, (mlokole) ni wale wanaojiita wasafi kwa jina la Yesu, huyo mama kila mwezi au wiki tatu hubadilisha mfanyakazi au wanaacha kazi kwa mateso yake. Sasa jee huyu mlokole anashinda kanisani kusali mpaka ndoa zinavunjika, hivyo tumuweke kundi gani? Mbona hawasemi “wanasali siku nzima na makelele mtaani na ni hao hao wanatesa wafanyakazi!” Jamani tuishi kwa kusema ukweli kuwa fitina za uzushi ni mbaya na haupiti muda huwarudia mwenyewe.

Kuna na mwengine ambaye anasema ni Mkenya anayedai kuwa alitaka kuuliwa na waliomuajiri Oman ili akawe kafara kwa mizimu ya Oman. Naye huyu ni mzushi mkubwa na unauona uzushi wake mara moja ukiwa si mtepetevu wa akili na unaweza kupima anayoyasema. Hebu hapa tutumie akili zetu kuchambua aliyoyasema:

Kwanza, anatuambia anakijua Kiarabu vizuri sana bila ya kututolea ushahidi. Lakini, tumkubalie kwa hili.

Pili, eti amewasikia waajiri wake wakipanga njama za kumuuwa ili kumtoa muhanga na akawasikia vizuri; hivyo kweli waajiri hao wapange njama zao mbele yake naye anawasikia!?

Tatu, eti ameingia chumbani kwake na akafungua ‘air condition’ na kupanga mito kama kuwa yeye amelala na kutoroka asije akauliwa na kutolewa muhanga! Tunajuaje kama huu ni uwongo? Jawabu: Waarabu hawakuwa na mila ya kumtoa binadamu muhanga hata katika siku hizo za ujahiliya kabla ya Uislamu, itakuwa leo!? Hii ni mila yao wenyewe baadhi ya Waafrika na anataka kuipandikiza kwa Waarabu! Tafuteni uzushi mwingine, huu hautafaa.

Nne, eti ametaka ubalozi wa Kenya kumsaidia na hawakumsaidia. Wakatae kumsaidia kwa sababu gani? Anasema haya ili tukitaka kuujua ukweli kutokana na Ubalozi tusiweze kuupata. Kwa nini? Kwa sababu anayoyasema si ya kweli kwani kesi zote zinazofikishwa balozini kokote duniani husajiliwa na hatua huchukuliwa na ubalozi. Huyu mzushi sura zake tumeshaziona, sasa na atuoneshe paspoti yake na mihuri ya kuingia na kutoka Oman na viza yake ya kufanya kazi Oman kama mkweli, tutaifuatilia kesi yake.

Tano, kwa vile waajiri wameshafikwa na mengi kutokana na waajiriwa, kuna walioibiwa dhahabu za kina mama, makarani waliofyeka pesa benki na kadhalika na kadhalika, ndio maana waajiri hao huchukua paspoti na kuziweka wao na kumpa mfanyakazi anapotaka kusafiri kihalali; mfanyakazi huwa na kadi tu. Sasa huyo mzushi, paspoti ya kusafiria aliipata wapi? Tiketi alimlipia nani?

Sita, hapana shaka, hata angelikuwanayo paspoti, hapana shaka ilichukua muda kabla ya kuweza kusafiri, hivyo siku ya pili asubuhi waajiri wake walipokuwa hawamuoni, unafikiri nini wangefanya awali? Si wangelipiga ripoti polisi kuwa mtumishi wao haonekani! Unafikiri polisi hufanya nini? Si hupeleka habari katika kila kituo cha usafiri. Na wakishapiga ripoti na popote atakapotaka kuondokea lazima wangelimzuia na wangelimuhoji na kama ana kesi ya kuwashitaki waajiri wake, basi kesi ingelifunguliwa na waajiri kushtakiwa. Sasa huyu mzushi ameondoka vipi Oman!

Nimekuandikieni haya kwa muhtasari tu. Mkifikiria vizuri mtagundua kuna hoja nyinginezo zinalifanya porojo hili kuwa la ki-paukwa pakawa. Hivyo basi, mkipanga njama zenu wazushi wa fitina tumieni akili, kama mnazo!

Mwishoni nasema kuwa wafanyakazi wa majumbani walioko Oman wanatoka kila mahala duniani. Idadi ya Wafilipino peke yake ni kubwa kwa mara nyingi sana kuliko ya Watanzania na huwasikii ila wachache sana kulalamika. Lakini idadi ya walalamikaji kutoka Tanzania ndiyo iliyo kubwa kabisa ingawa jumla yao ni ndogo sana Oman. Waomani hawana shida ya wafanyakazi. Wala hawatapungukiwa wala kuharibikiwa iwapo wafanyakazi kutoka Tanzania watazuiliwa kwenda kufanya kazi Oman. Sasa kazi kwetu. Kusuka au kunyoa.

WANAOSHANGAA Tanzania Kuomba Afrika Kusini Msaada Huenda Wakawa Hawajui Haya



Sasa mnashangaa nini Tanzania kuomba Afrika ya Kusini.

Hivi mmesahau jinsi tulivyowasaidia hawa tena buree.

Tuliwapa ofisi.

Tulwalipa mishahara.

Tukatoa jeshi letu kuwafundisha mapigano.

Tuliwapa silaha za kivita , magari ,vifaru.

Walikula ng'ombe wetu na kuku wetu.

Wakaoa na kuzaa na dada zetu.

Kiufupi Uhuru wao tumeutengeneza sisi Tanzania.

Tulitoa fedha za Watanzania kwa ajili ya ukombozi wa ndugu zao wa Afrika ya Kusini.

Leo isiwe nongwa , acheni watulipe fadhila kwa wema tuliowatendea.

Mahusiano na yadumu. 

Afrika ni moja na itabakia kua moja .

By Chiwinga A.

Rufaa Dhidi Ya Mbunge Wa Bunda Mjini Ester Bulaya Yafika Mahakama Ya Rufaa Jijiji Dares Salaam

Aliyekuwa  kuwa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Steven  Wassira  akiwa katika jengo la Mahakama ya Rufaa jijiji Dares Salaam akizungumza jambo na baadhi ya mawakili kabla ya kusikiliza kwa Rufaa ya kesi yake dhidi ya Mbunge wa Bunda mjini Ester Bulaya.  Katika kesi hiyo jopo la majaji watatu  wa Mahakama ya Rufaa limepanga kuendelea na kesi hiyo Jumatatu ijayo ya Aprili 15, mwaka huu. Uamuzi huo umetolewa  leo  Aprili 11, mwaka huu katika Mahakama hiyo  baada ya  Pande zote mbili  kutoa maelezo  ya sababu za rufaa. 

 Wakili wa Mbunge  wa Jimbo la Bunda Mjini, Tundu Lissu  akizungumza  jambo na mara baada kikao kilichokuwa kinasikiliza ombi la rufaa lilifunguliwa na  wapigakura wanne wa Jimbo la Bunda, kupinga  hukumu ya  Mahakama Kuu Kanda ya  Mwanza, kuhusu ushindi wa mbunge wa jimbo hilo, Ester Bulaya. 

Wakili  Constantine  Mutalemwa  akifafanua  jambo kwa baadhi  ya waandishi  wa habari  mara baada kikao kilichokuwa kinasikiliza ombi la rufaa lilifunguliwa na  wapigakura wanne wa Jimbo la Bunda, kupinga  hukumu ya  Mahakama Kuu Kanda ya  Mwanza, kuhusu ushindi wa mbunge wa jimbo hilo, Ester Bulaya.

WANAOSHANGAA Tanzania Kuomba Afrika Kusini Msaada Huenda Wakawa Hawajui Haya



Sasa mnashangaa nini Tanzania kuomba Afrika ya Kusini.

Hivi mmesahau jinsi tulivyowasaidia hawa tena buree.

Tuliwapa ofisi.

Tulwalipa mishahara.

Tukatoa jeshi letu kuwafundisha mapigano.

Tuliwapa silaha za kivita , magari ,vifaru.

Walikula ng'ombe wetu na kuku wetu.

Wakaoa na kuzaa na dada zetu.

Kiufupi Uhuru wao tumeutengeneza sisi Tanzania.

Tulitoa fedha za Watanzania kwa ajili ya ukombozi wa ndugu zao wa Afrika ya Kusini.

Leo isiwe nongwa , acheni watulipe fadhila kwa wema tuliowatendea.

Mahusiano na yadumu. 

Afrika ni moja na itabakia kua moja .

By Chiwinga A.

TUHUMA za Mateso Dhidi ya Wafanyakazi wa Ndani Oman, Mtanzania Afunguka Makubwa


Wafanyakazi wa majumbani walioko Oman wanatoka kila mahala duniani. Wafilipino peke yao ni wengi mara nyingi sana kuliko Watanzania na huwasikii ila wachache sana kulalamika. Lakini idadi ya walalamikaji kutoka Tanzania ndiyo iliyo kubwa kabisa ingawa jumla yao ni ndogo sana Oman.

Wapendwa waungwana na wapenda ukweli. Siku hizi za karibuni kumekuwako na upotoshwaji mkubwa wa habari za wafanyakazi wa ndani nchini Oman. Jamani waungwana, Waswahili husema kunya anye kuku akinya bata huambiwa kaharisha. Hizo habari za mayaya Oman ni za fitina na uchochezi uliokithiri na hazitamsaidia mtu yoyote, maana sisi ndio wahitaji zaidi wa hizo ajira nje ya nchi yetu.

Nchi za GCC zimekuwa na utaratibu wa miaka mingi kuajiri wafanyakazi kutoka nchi za Asia. Kwa kuzingatia msemo “mfae nduguyo kwanza” ndipo Waomani wakawa pia na utaratibu wa kuwaajiri wafanyakazi kutoka Afrika Mashariki, kwa kuwa kuna historia ya muda mrefu na ya kidugu baina yao. Sasa imekuwa balaa kila kukicha ni matusi yasiyokuwa na maana ila kutapakaza fitina na chuki kwenye mitandao ya kijamii na hata baadhi ya vyombo vya habari kama vile magazeti na televisheni.

Bora nitangulize kusema kitu kimoja ambacho mtu yeyote mwenye akili zake timamu na kupenda kusikia ukweli hawezi kukikataa, nacho ni kuwa hakuna nchi yoyote duniani ambayo haina watu wema na pia watu waovu. Mambo ni kuzidiana tu. Wala hakuna nchi yenye matajiri wenye kuajiri wafanya kazi pasitokee wenye kudhulumu na wenye kudhulumiwa. Kwa vile nazijua vizuri nchi mbili hizi — Tanzania na Oman — naweza pia kusema kwa uhakika kuwa baina ya Tanzania na Oman, utakuta kuwa dhulma wanazotendewa wafanyakazi wa majumbani Tanzania ni kubwa zaidi ukilinganisha na Oman.

Hapa Tanzania wapo wafanyakazi wanaoteseka kila siku na jamaa zao wenyewe kwa mshahara wa shilingi 20,000 au 40,000 kwa mwezi. Sio hilo tu la mshahara, bali hata siku za mapumziko za Jumamosi na Jumapili au zile sikukuu za kitaifa, hawapewi. Haya ni ya ukweli kabisa na wala sio siri. Ukitaka kumtoa mtu kijiti jichoni mwake, kwanza jiangalie kama jicho lako halina boriti.

Hapa Tanzania wafanyakazi wana kila mateso lakini wanavumilia tu. Ukifuatilia kwa makini utagundua kuwa haya ya uchochezi uliojaa fitina unatokana na kundi fulani ambalo hawapendelei pawe na masikilizano mema baina ya Waarabu na Waafrika. Na lengo lao hasa hata si Waarabu. Ukipeleleza kwa makini utagundua kuwa wanachokichukia kweli ni dini waliyoileta Waarabu, nayo ni Uislamu.

Katika siku za hivi karibuni kuna sauti zinatumwa na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii, hasa WhatsApp na Instagram, zikidai kuwa kuna wafanyakazi wa majumbani nchini Oman wanateswa vibaya hadi kusema kuwa wanauawa kwa makusudi na wengine wanapangiwa njama za kuuliwa ili wawe mihanga kwa majini ya Kiomani. Mojawapo ni sauti ya mama mtu mzima ambaye dhahiri kabisa inaonekana kuwa alitumwa kusudi kutukana dini ya Kiislamu.

Hilo ndilo lengo lao hasa, maana hakuwa na haja ya kutaja maneno kama vile kuwa watu wanasali sala tano kila siku halafu wanatesa watu. Hiyo haikuhusu kabisa. Ikiwa sala tano zinawaudhi basi wataumia sana. Mimi binafsi nimeishi na Mlokole wa Kanisa la Efatah, (mlokole) ni wale wanaojiita wasafi kwa jina la Yesu, huyo mama kila mwezi au wiki tatu hubadilisha mfanyakazi au wanaacha kazi kwa mateso yake. Sasa jee huyu mlokole anashinda kanisani kusali mpaka ndoa zinavunjika, hivyo tumuweke kundi gani? Mbona hawasemi “wanasali siku nzima na makelele mtaani na ni hao hao wanatesa wafanyakazi!” Jamani tuishi kwa kusema ukweli kuwa fitina za uzushi ni mbaya na haupiti muda huwarudia mwenyewe.

Kuna na mwengine ambaye anasema ni Mkenya anayedai kuwa alitaka kuuliwa na waliomuajiri Oman ili akawe kafara kwa mizimu ya Oman. Naye huyu ni mzushi mkubwa na unauona uzushi wake mara moja ukiwa si mtepetevu wa akili na unaweza kupima anayoyasema. Hebu hapa tutumie akili zetu kuchambua aliyoyasema:

Kwanza, anatuambia anakijua Kiarabu vizuri sana bila ya kututolea ushahidi. Lakini, tumkubalie kwa hili.

Pili, eti amewasikia waajiri wake wakipanga njama za kumuuwa ili kumtoa muhanga na akawasikia vizuri; hivyo kweli waajiri hao wapange njama zao mbele yake naye anawasikia!?

Tatu, eti ameingia chumbani kwake na akafungua ‘air condition’ na kupanga mito kama kuwa yeye amelala na kutoroka asije akauliwa na kutolewa muhanga! Tunajuaje kama huu ni uwongo? Jawabu: Waarabu hawakuwa na mila ya kumtoa binadamu muhanga hata katika siku hizo za ujahiliya kabla ya Uislamu, itakuwa leo!? Hii ni mila yao wenyewe baadhi ya Waafrika na anataka kuipandikiza kwa Waarabu! Tafuteni uzushi mwingine, huu hautafaa.

Nne, eti ametaka ubalozi wa Kenya kumsaidia na hawakumsaidia. Wakatae kumsaidia kwa sababu gani? Anasema haya ili tukitaka kuujua ukweli kutokana na Ubalozi tusiweze kuupata. Kwa nini? Kwa sababu anayoyasema si ya kweli kwani kesi zote zinazofikishwa balozini kokote duniani husajiliwa na hatua huchukuliwa na ubalozi. Huyu mzushi sura zake tumeshaziona, sasa na atuoneshe paspoti yake na mihuri ya kuingia na kutoka Oman na viza yake ya kufanya kazi Oman kama mkweli, tutaifuatilia kesi yake.

Tano, kwa vile waajiri wameshafikwa na mengi kutokana na waajiriwa, kuna walioibiwa dhahabu za kina mama, makarani waliofyeka pesa benki na kadhalika na kadhalika, ndio maana waajiri hao huchukua paspoti na kuziweka wao na kumpa mfanyakazi anapotaka kusafiri kihalali; mfanyakazi huwa na kadi tu. Sasa huyo mzushi, paspoti ya kusafiria aliipata wapi? Tiketi alimlipia nani?

Sita, hapana shaka, hata angelikuwanayo paspoti, hapana shaka ilichukua muda kabla ya kuweza kusafiri, hivyo siku ya pili asubuhi waajiri wake walipokuwa hawamuoni, unafikiri nini wangefanya awali? Si wangelipiga ripoti polisi kuwa mtumishi wao haonekani! Unafikiri polisi hufanya nini? Si hupeleka habari katika kila kituo cha usafiri. Na wakishapiga ripoti na popote atakapotaka kuondokea lazima wangelimzuia na wangelimuhoji na kama ana kesi ya kuwashitaki waajiri wake, basi kesi ingelifunguliwa na waajiri kushtakiwa. Sasa huyu mzushi ameondoka vipi Oman!

Nimekuandikieni haya kwa muhtasari tu. Mkifikiria vizuri mtagundua kuna hoja nyinginezo zinalifanya porojo hili kuwa la ki-paukwa pakawa. Hivyo basi, mkipanga njama zenu wazushi wa fitina tumieni akili, kama mnazo!

Mwishoni nasema kuwa wafanyakazi wa majumbani walioko Oman wanatoka kila mahala duniani. Idadi ya Wafilipino peke yake ni kubwa kwa mara nyingi sana kuliko ya Watanzania na huwasikii ila wachache sana kulalamika. Lakini idadi ya walalamikaji kutoka Tanzania ndiyo iliyo kubwa kabisa ingawa jumla yao ni ndogo sana Oman. Waomani hawana shida ya wafanyakazi. Wala hawatapungukiwa wala kuharibikiwa iwapo wafanyakazi kutoka Tanzania watazuiliwa kwenda kufanya kazi Oman. Sasa kazi kwetu. Kusuka au kunyoa.

Mvua Sababisha Maporomoko ya Mawe Tanga..Barabara ya Dar Arusha Yafungwa

Jeshi la Polisi mkoani Tanga imefunga barabara ya kutokea Dar es salaam kuelekea Arusha kufuatia eneo la Mombo mkoani Tanga kuangukiwa na maporomoko ya mawe pamoja na matope na kusababisha athari kwa baadhi ya magari

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi mkoani humo Benedict Wakuyamba  amesema, maporomoko hayo yamesababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Mkoani humo na maeneo mbalimbali nchini

"Hali ya mvua imeendelea kunyesha na kufukia barabara eneo la Mombo kutokea Dar es salaam kuelekea Arusha ambapo matope na miti vimesombwa na kukwama barabarani hali iliyokwamisha magari makubwa kwa madogo kusafiri kupitia eneo hilo..Niwaombe abiria au wananchi kwa ujumla kama hawana ulazima wa kusafiri kwenda mikoa ya Kaskazini ni vizuri wakatulia kwa siku mbili tuone hali inakwendaje kwa ajili ya usalama wao". Alisema Kamishna Msaidizi Benedict

Kwa upande mwingine Kamishna huyo amesema TANROADS na Jeshi la Polisi mkoani humo wanaendelea kusaidia kuondoa magogo na tope zilizosakama katika barabara ili kunusuru hali ya usafiri

 

Gallery

Popular Posts

About Us